Sababu Gani Tuondoke Mara Moja?
Wakati tunakutana na ndugu zetu kwenye mukutano kwa ajili ya mahubiri, kwa kawaida tunapenda kuzungumuza nao. Hata hivyo, kisha tu mukutano kwa ajili ya mahubiri, tunapaswa kuondoka mara moja na kuenda katika eneo. Kazi ya kuhubiri ni ya kufanywa kwa haraka. (2 Tim. 4:2) Ikiwa hatuondoke mara moja, tutapitisha wakati mudogo katika mahubiri. Tutakuwa na nafasi nyingi za kufurahia urafiki wenye kujenga pamoja na wahubiri wenzetu wakati tunatoka nao katika mahubiri. Kuondoka bila kupoteza wakati kisha mukutano kwa ajili ya mahubiri, kutaonyesha kwamba tunamutumikia Yehova na Mwana wake kwa moyo wote.—Rom. 12:11.