Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 9/15 uku. 3
  • Kufundisha kwa Kutumia Broshua Habari Njema

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Kufundisha kwa Kutumia Broshua Habari Njema
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2015
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Namna ya Kutumia Broshua Habari Njema Inayotoka kwa Mungu!
    Huduma Yetu ya Ufalme—2013
  • Namna ya Kuongoza Funzo kwa Kutumia Broshua Habari Njema
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2016
  • Tuanzishe Mafunzo ya Biblia Katika Broshua Anataka
    Huduma Yetu ya Ufalme—1999
  • Tumtegemee Yehova ili ‘Kufululiza Kukuza’
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2015
km 9/15 uku. 3

Kufundisha kwa Kutumia Broshua Habari Njema

1. Broshua Habari Njema imeandikwa namna gani?

1 Kama vile tuliona katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Mwezi wa 7, broshua Habari Njema Inayotoka kwa Mungu! ni chombo kizuri sana cha kufundisha chenye hakipaswe kukosa katika sakoshi yetu ya mahubiri. Maandiko yote yenye kuwa katika broshua hiyo hayatajwe; muyasome katika Biblia. Vitabu vingine vya funzo vimeandikwa kwa njia yenye mutu anaweza kuvielewa mwenyewe; lakini broshua hii imeandikwa ili mazungumuzo yaongozwe na mwalimu. Kwa hiyo, wakati tunatolea mutu broshua hii, tujikaze kumuonyesha namna tunajifunza Biblia na watu ili ajionee mwenyewe namna kujifunza habari njema ya Biblia kunavutia sana.—Mat. 13:44.

2. Namna gani unaweza kutumia broshua Habari Njema wakati unamutembelea mutu kwa mara ya kwanza?

2 Wakati Unamutembelea Mutu kwa Mara ya Kwanza: Unaweza kusema hivi: “Ninakutembelea kwa sababu watu wanajiuliza sana kama maisha itakuwa namna gani wakati wenye kuja. Unawaza hali ya watu itakuwa muzuri zaidi? [Acha mutu ajibu.] Biblia iko na habari njema yenye kutupatia tumaini. Ona maulizo fulani yenye Biblia inajibia.” Umupatie broshua, na umualike achague ulizo moja kwenye ukurasa wa mwisho wa broshua. Kisha, umuonyeshe namna funzo linafanywa kwa kuchunguza fungu la kwanza la somo lenye alichagua. Njia ingine ni kuuliza musikilizaji ulizo fulani lenye kutegemea somo lenye unataka na kisha umuonyeshe namna broshua hii inaweza kumusaidia apate jibu la Biblia. Kama somo hilo linatapana na video fulani kwenye jw.org, wahubiri fulani wanaonyesha video hiyo mutu mwenye wanatolea ujumbe.

3. Eleza namna unaweza kuongoza funzo kupitia broshua Habari Njema.

3 Namna ya Kuongoza Funzo: (1) Soma ulizo nyeusi lenye kuanza na namba ili kumusaidia musikilizaji akazie uangalifu wazo kubwa. (2) Soma fungu lenye kuwa chini ya ulizo hilo. (3) Soma maandiko yenye kuwa na neno “Soma”, na uliza maulizo mengine ili kumusaidia musikilizaji apate jibu la ulizo nyeusi lenye kuanza na namba. (4) Kama kuna fungu lingine, rudilia maagizo yenye kuwa kwenye nukta ya 2 na 3. Kama video fulani inajibia ulizo hilo na kama musikilizaji hajaiona, unaweza kuionyesha wakati fulani wa mazungumuzo. (5) Kwa mwisho, uliza tena musikilizaji ulizo nyeusi lenye kuanza na namba ili uhakikishe kwamba ameelewa.

4. Ni nini itakusaidia ukuwe na uzoefu wa kutumia broshua Habari Njema?

4 Ujikaze kujua muzuri habari zenye kuwa ndani ya broshua hii. Tumia broshua hii kila wakati nafasi inajitokeza. Mbele ya kila funzo, ufikiri sana juu ya mwanafunzi na ili ufikiri naye muzuri, tumia maandiko yenye kuwa katika somo lenye mutajifunza. (Met. 15:28; Mdo. 17:2, 3) Wakati utakuwa na ufundi na uzoefu wa kutumia broshua hiyo, utaona kwamba ni chombo kizuri sana cha kutumia ili kufundisha watu kweli!

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine