IKualika watu kwenye Chakula cha Bwana cha Mangaribi katika inchi ya Albania
Namna ya Kuanzisha Mazungumuzo
MUNARA WA MULINZI
Ulizo: Unawaza Mungu ametupatia zawadi gani kubwa?
Andiko: Yoh 3:16
Namna ya kutoa: Gazeti hii inaonyesha sababu gani Mungu alituma Yesu mu dunia akufe kwa ajili yetu na namna tunaweza kuonyesha shukrani yetu kwa zawadi hiyo.
UFALME WA MUNGU NI NINI?
Ulizo: [Onyesha musikilizaji ukurasa wa kwanza wa trakte.] Unachagua jibu gani? Ufalme wa Mungu ni hali ya moyo? Ni usemi wa mufano tu? Ao ni serikali ambayo iko mbinguni?
Andiko: Dan 2:44; Isa 9:6
Namna ya Kutoa: Trakte hii inaeleza mambo yenye Ufalme wa Mungu utakufanyia.
MUALIKO KWA AJILI YA UKUMBUSHO
Namna ya Kutoa: Tunakuletea mualiko wako! [Mupatie mualiko.] Tarehe 11 Mwezi wa 4, mu dunia yote watu wengi sana watakusanyika ili kukumbuka kifo cha Yesu na kusikiliza hotuba yenye kutegemea Biblia ambayo itaonyesha faida yenye kifo hicho kinatuletea. Kuingia ni bure. Mahali na saa vinapatikana kwenye mualiko wako. Tutafurahi kukuona.
ANDIKA NAMNA UNAWEZA PIA KUANZISHA MAZUNGUMUZO
Ulizo:
Andiko:
Namna ya Kutoa: