MAISHA YA MUKRISTO
Kuchunguza Maandiko Kila Siku Kunakuletea Faida Gani?
Kusoma andiko la Biblia na mafasirio yenye kuwa katika broshua Tuchunguze Maandiko Kila Siku ni kati ya mambo ya kiroho yenye unafanyaka kila siku ili kumukaribia Yehova? Kama haufanyake vile, unaweza kuongeza ile programu mu mambo yenye unafanyaka kila siku? Watu mingi wanachunguzaka andiko la siku asubuhi ili wafikiri juu ya mawazo yenye walisoma wakati wako wanafanya mambo mbalimbali. (Yos 1:8; Zb 119:97) Unaweza kufanya nini ili kupata faida zaidi kwa kuchunguza Andiko la siku? Soma mistari yenye kuzunguka Andiko la Biblia ili uelewe ni wakati gani na ni katika hali gani mambo ilifanyika. Jaribu kufikiria habari fulani ya Biblia yenye kuzungumuzia kanuni yenye inakaziwa katika andiko. Kisha, ufikirie namna unaweza kutumikisha ile kanuni mu maisha yako. Wakati unatumia Biblia ili kukamata maamuzi, itaongoza maisha yako na itakuletea faida kabisa.—Zb 119:105.
Mu dunia yote, familia za Beteli zinachunguzaka andiko wakati wa chakula cha asubui. Kuanzia miaka fulani yenye imepita, mazungumuzo mingi ya ile programu inaendelea kuwekwa kwenye JW Télédiffusion® chini ya sehemu MATUKIO NA HOTUBA. Ni wakati gani uliangalia tena zile programu kwa mara ya mwisho? Pengine habari fulani yenye kuwa mu zile programu njo yenye uko nayo lazima kabisa. Kwa mufano, namna gani habari ya Loti inaweza kukusaidia wakati uko unakamata maamuzi?
MUANGALIE VIDEO MUSIPENDE ULIMWENGU (1YO 2:15), KISHA MUJIBIE MAULIZO YENYE KUFUATA:
Ile Ibada ya Asubui ilitegemea zaidi kanuni gani ya Biblia?
Namna gani habari ya Loti inaonyesha hatari ya kupenda ulimwengu ao vitu vyenye kuwa katika ulimwengu?—Mwa 13:12; 14:12; 19:3, 12, 13, 24-26
Namna gani tunaonyesha kama tunamupenda Yehova hapana ulimwengu ao vitu vyenye kuwa katika ulimwengu?
Namna gani ninaweza kuonyesha kila siku kama ninaona Neno la Yehova kuwa la maana?