Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • g16 na. 4 uku. 5
  • 2 Epuka Hali Zenye Zinaweza Kukuletea Magumu

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • 2 Epuka Hali Zenye Zinaweza Kukuletea Magumu
  • Amuka!—2016
  • Habari za Kufanana na Zile
  • 1 Ukuwe Mwenye Kiasi
    Amuka!—2016
  • Utangulizi
    Amuka!—2016
  • Utangulizi
    Amuka!—2017
  • Namna ya Kuwa na Uwezo Juu ya Tabia Zako
    Amuka!—2016
Ona Habari Zaidi
Amuka!—2016
g16 na. 4 uku. 5
Nguo za kufanya nazo mazoezi, viatu, chupa ya maji, na chombo cha kielektroniki vinatayarishwa usiku kwa ajili ya mazoezi

HABARI KUBWA | NAMNA YA KUWA NA UWEZO JUU YA TABIA ZAKO

2 Epuka Hali Zenye Zinaweza Kukuletea Magumu

  • Uliamua kuanza kula chakula cha muzuri zaidi, lakini inaonekana kama kreme ya baridi inakuvutia sana.

  • Uliamua kuacha kuvuta tumbako, lakini rafiki yako mwenye anajua kwamba unajikaza kuacha kuvuta, anakupatia tena tumbako.

  • Uliamua kufanya mazoezi leo, lakini wakati unatafuta viatu vya kukimbia navyo nafasi kwenye unawekea vitu, inaonekana kuwa ni kazi kubwa!

Hali hizo zinafanana katika njia gani? Mara nyingi, imeonekana kwamba mazingira yetu, ni kusema, hali zenye tunaishi ndani na watu wenye tunaishi nao, yanaweza kutusaidia kuacha tabia za mubaya na kuwa na tabia za muzuri.

KANUNI YA BIBLIA: ‘Mutu mwerevu ni yule ambaye ameona musiba na kujificha, lakini wasio na uzoefu wameendelea mbele nao lazima waumie.’—Methali 22:3.

Biblia inatushauri kuona mambo yenye kuwa mbele. Kwa kufanya hivyo, tunaweza kuepuka hali zenye zinaweza kufanya tushindwe kutimiza mipango yetu, na kwa hiyo kutusaidia tukuwe katika hali za muzuri zaidi. (2 Timotheo 2:22) Kwa kifupi, ni jambo la hekima kuepuka hali zenye zinaweza kukuletea magumu.

Ujikaze ikuwe nguvu sana kufanya jambo fulani la mubaya na mwepesi sana kufanya jambo la muzuri

MAMBO UNAWEZA KUFANYA

  • Ujikaze ikuwe nguvu sana kufanya jambo fulani la mubaya. Kwa mufano, kama haupendi kula chakula chenye hakifae, ujikaze kuepuka kutia chakula hicho katika mafiga. Hilo litafanya ikuwe nguvu zaidi kula chakula hicho wakati unajikuta katika jaribu la kutaka kufanya hivyo.

  • Ujikaze ikuwe mwepesi sana kufanya jambo la muzuri. Kwa mufano, kama unapanga kufanya mazoezi ya mwili asubui, utie mavazi ya kufanya nayo mazoezi pembeni ya kitanda chako mbele ya kulala. Kama inakuwa mwepesi kuanza kufanya jambo fulani, inaweza kuwa pia mwepesi kuendelea kulifanya.

  • Uchague marafiki wazuri. Mara nyingi tunafuata mufano wa watu wenye tunapitisha nao wakati. (1 Wakorintho 15:33) Kwa hiyo, ujikaze kuepuka watu wenye watakutia moyo ukuwe na tabia zenye unapenda kuacha, na utafute watu wenye watakusaidia uonyeshe muzuri zaidi tabia za muzuri.

KANUNI ZINGINE ZA BIBLIA

“Anayetembea na watu wenye hekima atakuwa na hekima.”—Methali 13:20.

‘Mipango ya mwenye bidii bila shaka inaleta faida.’—Methali 21:5.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine