Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • bt sura 23 uku. 181-188
  • “Musikilize . . . Namna Ninajitetea”

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • “Musikilize . . . Namna Ninajitetea”
  • “Kutoa Ushahidi Kamili” juu ya Ufalme wa Mungu
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • “Wakaanza Kumutukuza Mungu” (Mdo. 21:18-20a)
  • Wengi Walikuwa Wangali “Wenye Bidii kwa Ajili ya Sheria.” (Mdo. 21:20b, 21)
  • “Habari Zenye Waliambiwa Juu Yako Haziko za Kweli” (Mdo. 21:22-26)
  • “Hastahili Kuishi!” (Mdo. 21:27–22:30)
  • “Mimi Ni Mufarisayo” (Mdo. 23:1-10)
  • Ukuwe Hodari​—Yehova Ni Musaidizi Wako
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2020
  • “Kutoa Ushahidi Kamili”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” juu ya Ufalme wa Mungu
  • “Niko Safi Kutokana Na Damu ya Watu Wote”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” juu ya Ufalme wa Mungu
  • Maulizo ya Wasomaji Wetu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2021
“Kutoa Ushahidi Kamili” juu ya Ufalme wa Mungu
bt sura 23 uku. 181-188

SURA YA 23

“Musikilize . . . Namna Ninajitetea”

Paulo anatetea imani yake mbele ya vikundi vya watu wenye kasirani na mbele ya Sanhedrini

Inategemea Matendo 21:18–23:10

1, 2. Juu ya nini Paulo alienda Yerusalemu, na alipambana na matatizo gani kule?

PAULO iko tena Yerusalemu! Iko natembea mu barabara za Yerusalemu za kidogo zenye kuyala watu wengi. Mu dunia yote hakuna muji wenye kuzungumuziwa sana kuhusiana na ibada ya kweli sawa vile Yerusalemu. Watu wengi kule walijivunia historia ya taifa yao. Paulo anajua kama Wakristo wengi wa Yerusalemu wanakazia sana namna yao ya kuabudu ya zamani, kuliko kujipatanisha na namna ya mupya ya kuabudu yenye Yehova alikuwa nawafundisha. Kwa hiyo, wakati Paulo alikuwa Efeso alipanga kuenda Yerusalemu. Kusudi yake haikukuwa tu kupelekea ndugu wa Yerusalemu michango, lakini pia kuwasaidia wabadilishe mawazo yao. (Mdo. 19:21) Aliamua kuenda Yerusalemu hata kama ilikuwa hatari kufanya vile.

2 Paulo atapambana na mambo gani Yerusalemu? Tatizo moya ilikuwa hii: Ndugu fulani waliamini habari za uongo kumuhusu Paulo. Na tatizo kubwa zaidi ilitoka kwa maadui wa Kristo. Walisingizia Paulo mambo ya uongo, walimupiga, na wakamuogopesha kama watamuua. Ile yote ilipatia Paulo nafasi ya kutetea imani yake. Paulo alipambana na ile magumu yote kwa unyenyekevu, kwa uhodari, na kwa imani. Alituachia mufano muzuri. Tuone namna gani.

“Wakaanza Kumutukuza Mungu” (Mdo. 21:18-20a)

3-5. (a) Paulo alihuzuria mukutano gani katika Yerusalemu, na walizungumuzia nini? (b) Mukutano wenye Paulo alifanya pamoya na wazee unaweza kutufundisha nini?

3 Siku yenye ilifuata kisha Paulo na wenzake kufika Yerusalemu, walienda kuonana na wazee wenye walikuwa naongoza kutaniko. Mu hii habari, Biblia haitaye hata mutume mumoja; pengine wote walikuwa wameenda kutumikia mu maeneo ingine. Lakini, Yakobo ndugu ya Yesu alikuwa angali Yerusalemu. (Gal. 2:9) Inawezekana, Yakobo njo alisimamia mukutano wakati “wazee wote walikuwa pale” pamoja na Paulo.​—Mdo. 21:18.

4 Paulo alisalimia wazee “na kuanza kuwaelezea kwa urefu mambo yenye Mungu alifanya katikati ya mataifa kupitia utumishi wake.” (Mdo. 21:19) Na bila shaka walitiwa moyo sana. Leo pia tunatiwa moyo sana wakati tunasikia maendeleo ya kazi ya kuhubiri mu inchi zingine.​—Mez. 25:25.

5 Wakati fulani mu ile mazungumuzo, pengine Paulo alizungumuzia kuhusu michango yenye alileta kutoka mu maeneo ya Ulaya. Bila shaka wale ndugu waliguswa moyo sana wakati walijua kama ndugu zao wa mu maeneo ya mbali waliwahangaikia kabisa. Kwa hiyo, wakati wazee walisikia mambo yote yenye Paulo aliwaelezea, “wakaanza kumutukuza Mungu”! (Mdo. 21:20a) Leo pia, ndugu na dada wenye wanateseka kwa sababu ya misiba ao magonjwa wanaguswa moyo sana wakati waamini wenzao wanawatumia misaada na kuwatia moyo kupitia maneno yao.

Wengi Walikuwa Wangali “Wenye Bidii kwa Ajili ya Sheria.” (Mdo. 21:20b, 21)

6. Paulo alijulishwa kuhusu tatizo gani?

6 Kisha wazee wakaambia Paulo kama Yudea kulikuwa tatizo yenye ilimuhusu. Walimuambia hivi: “Ndugu, unaona namna kuko maelfu ya Wayahudi wenye wamekuwa waamini, na wote ni wenye bidii kwa ajili ya Sheria. Lakini wamesikia habari fulani juu yako kwamba wewe umekuwa ukifundisha Wayahudi wote kati ya mataifa kuacha Sheria ya Musa, ukiwaambia wasitahiri watoto wao na wasifuate desturi za kawaida.”a​—Mdo. 21:20b, 21.

7, 8. (a) Wakristo wengi Wayahudi walikuwa na mawazo gani yenye makosa? (b) Kuwa na ile mawazo, kulifanya wasistahili tena kuwa Wakristo?

7 Juu ya nini Wakristo wengi waliendelea kuwa na bidii kwa ajili ya Sheria ya Musa, hata kama kulikuwa kumepita miaka zaidi ya 20 tangu ifikie mwisho? (Kol. 2:14) Mu 49 K.K.Y. mitume na wazee walikusanyika Yerusalemu na walituma barua kwa makutaniko na ilifasiria kama Watu wa Mataifa hawakulazimika kutahiriwa na kushika Sheria ya Musa. (Mdo. 15:23-29) Lakini, ile barua haikuzungumuzia Wakristo Wayahudi, wenye wengi kati yao hawakuelewa kama Sheria ya Musa haikukuwa natumika tena.

8 Ile mawazo ilifanya wale Wakriso Wayahudi wasistahili tena kuwa Wakristo? Hapana. Hata mbele wakuwe Wakristo hawakukuwa naabudu miungu ya kipagani na hawakukuwa nafuata desturi za dini ya uongo. Ile Sheria yenye waliona kuwa ya maana sana ni Yehova njo aliitowaka. Haikukuwa ya mashetani na haikukuwa ya mubaya. Lakini ile Sheria ilikuwa mu agano ya zamani, na sasa Wakristo walikuwa chini ya agano jipya. Yehova hakuwaomba tena watii ile Sheria ili awakubali. Wakristo Wayahudi wenye walikuwa wangali na bidii kwa ajili ya Sheria, hawakuelewa ao kutumainia kutaniko ya Kikristo. Walipaswa kupatanisha mawazo yao na kweli za mupya zenye Yehova alikuwa nawafundisha.b​—Yer. 31:31-34; Lu. 22:20.

“Habari Zenye Waliambiwa Juu Yako Haziko za Kweli” (Mdo. 21:22-26)

9. Paulo alifundisha nini kuhusu Sheria ya Musa?

9 Tuseme nini juu ya habari zenye watu walikuwa wanasema ya kama Paulo alikuwa nafundisha Wayahudi kati ya mataifa “wasitahiri watoto wao na wasifuate desturi za kawaida”? Paulo alikuwa mutume kwa Watu wa Mataifa, na aliwafasiria uamuzi wenye ulionyesha kama hawakulazimika kufuata Sheria ya Musa. Alionyesha kama ilikuwa kosa kulazimisha Wakristo wenye hawakukuwa Wayahudi watahiriwe ili kuonyesha kama wanatii Sheria ya Musa. (Gal. 5:1-7) Mu miji yenye alitembelea, Paulo alihubiria pia Wayahudi. Na ni wazi kama alifasiria Wayahudi wenye walimusikiliza kama kifo ya Yesu njo ilikuwa mwisho wa Sheria. Aliwafasiria pia kama haiko kufuata Sheria ya Musa njo ilifanya Mungu akubali mutu, lakini ni kuwa na imani.​—Ro. 2:28, 29; 3:21-26.

10. Paulo alikuwa na maoni gani yenye kusawazika kuhusu Sheria na kutahiriwa?

10 Hata vile, Paulo hakuhukumu Wayahudi fulani wenye walipenda kuendelea kufuata desturi fulani za Kiyahudi, sawa vile kuepuka kutumika siku ya Sabato ao kuepuka chakula fulani. (Ro. 14:1-6) Na hakutilia watu sheria kuhusu kutahiriwa. Na hata alimuambia Timoteo atahiriwe ili Wayahudi wasimukatale kwa sababu walijua kama baba yake alikuwa Mugiriki. (Mdo. 16:3) Kutahiriwa ao hapana ilikuwa uamuzi wa kipekee. Paulo aliambia hivi Wagalatia: “Kutahiriwa ao kutokutahiriwa hakuna faida yoyote lakini imani yenye inatenda kupitia upendo ndiyo iko na faida.” (Gal. 5:6) Lakini, ikiwa mutu angetahiriwa ili tu kutii Sheria ao angewaza kama kutahiriwa njo kungefanya akubaliwe na Mungu, ile ingeonyesha kama hana imani.

11. Wazee walipatia Paulo shauri gani, na kufanya vile kungetia ndani nini? (Ona pia maelezo ya chini.)

11 Hata kama zile habari kuhusu Paulo hazikukuwa za kweli, Wakristo Wayahudi walikwazika. Njo maana wazee walipatia Paulo hii shauri: “Tuko na wanaume ine (4) wenye walijiwekea wenyewe naziri. Chukua watu hawa na ujitakase pamoja nao kulingana na desturi na uwalipie mambo yenye wako nayo lazima, ili wanyolewe vichwa vyao. Kisha wote watajua kwamba habari zenye waliambiwa juu yako haziko za kweli, lakini unatembea kwa utaratibu na pia unashika Sheria.”c​—Mdo. 21:23, 24.

12. Namna gani Paulo alionyesha kama alikuwa tayari kufuata muongozo wa wazee?

12 Paulo angejitetea kwa kusema kama shida ilikuwa bidii ya Wayahudi kwa ajili ya Sheria ya Musa, hapana mambo yenye watu walikuwa nasema juu yake. Lakini alikuwa tayari kutii wazee wakati ile haikuvunja kanuni za Mungu. Mbele ya pale, alikuwa ameandika hivi: “Kwa wale wenye kuwa chini ya sheria nilikuwa kama mwenye kuwa chini ya sheria, hata kama mimi mwenyewe siko chini ya sheria, ili nipate wale wenye kuwa chini ya sheria.” (1 Ko. 9:20) Mu hii hali, Paulo alifuata muongozo wa wazee wa Yerusalemu na akakuwa “kama mwenye kuwa chini ya sheria.” Kwa kufanya vile, alituachia mufano muzuri. Siye pia tunapaswa kufuata muongozo wa wazee na kuepuka kukazia mawazo yetu.​—Ebr. 13:17.

Picha: 1. Paulo alifuata muongozo wa wazee katika Yerusalemu. 2. Leo ku mukutano wa wazee, ndugu mumoja anaangalia kwa uangalifu wakati wazee wenzake wanatia mukono juu.

Paulo alikubali kufuata muongozo wa wazee juu haukuvunja kanuni za Biblia. Na weye unakuwaka tayari kufanya vile?

SHERIA YA ROMA NA RAIA WA ROMA

Serikali ya Roma iliruhusu watawala wa maeneo yenye ilitawala wajikamatie maamuzi wao wenyewe. Kwa hiyo, mara mingi Wayahudi waliongozwa na sheria za Wayahudi. Waroma walijiingiza mu kesi ya Paulo juu fujo yenye ingetokea mu hekalu ingevuruga amani ya muji.

Kama mutu hakukuwa raia wa Roma hakukuwa na haki za mingi mu Utawala wa Roma. Lakini serikali ya Roma ilitendea raia wa Roma mu njia tofauti.f Raia wa Roma alikuwa na uhuru na haki zenye wengine hawakukuwa nazo na aliheshimiwa mu utawala wote. Kwa mufano kupiga na kufunga raia wa Roma mbele ahukumiwe ilikuwa kuvunja sheria. Ni watumwa tu njo wangetendewa vile. Raia wa Roma walikuwa pia na haki ya kukatala maamuzi ya gavana wa jimbo na kuomba kesi yao isikilizwe na mutawala katika Roma.

Mutu angeweza kupata uraia wa Roma mu njia mbalimbali. Kwanza mutu angeweza kuriti uraia wa Roma kutoka kwa wazazi wake. Wakati fulani watawala wangeweza kupatia mutu ao watu wote wenye kuishi mu muji ao jimbo fulani uraia wa Roma ili kuwashukuru kwa sababu ya jambo ya muzuri yenye walifanyia Utawala wa Roma. Ni watumwa tu wenye kuishi mu ile muji ao jimbo njo hawangepata uraia wa Roma. Mutumwa mwenye aliuza uhuru wake kutoka kwa raia wa Roma, mutumwa mwenye aliwekwa huru na Muroma, ao askari mwenye hakukuwa Muroma mwenye alipigania jeshi ya Roma mupaka wakati kazi yake ya kiaskari ilifikia mwisho, angeweza kuwa raia wa Roma. Inaonekana mu hali fulani iliwezekana kuuza uraia wa Roma. Kiongozi wa jeshi mwenye kuitwa Klaudio Lisia alimuambia hivi Paulo: “Mimi nilinunua haki hizi za kuwa raia kwa feza nyingi.” Paulo alimujibia hivi: “Lakini mimi nilizaliwa nazo.” (Mdo. 22:28) Kwa hiyo inawezekana mumoja kati ya mababu wa Paulo alipata uraia wa Roma, lakini hatujue kabisa kama aliupata namna gani.

f Mu karne ya kwanza kisha kuzaliwa kwa Yesu, mu Yudea hamukukuwa raia wengi wa Roma. Ni mu karne ya tatu njo watu wote wenye kuishi mu maeneo yenye kutawaliwa na Roma walipewa uraia wa Roma.

“Hastahili Kuishi!” (Mdo. 21:27–22:30)

13. (a) Juu ya nini Wayahudi fulani walianzisha fujo ku hekalu? (b) na Paulo aliokoka namna gani?

13 Mambo haikuendeka muzuri ku hekalu. Wakati siku ya kumaliza kutimiza naziri ilikaribia, Wayahudi kutoka Asia walimuona Paulo na kumushitaki mambo ya uongo. Walimushitaki kama alikuwa analeta Watu wa Mataifa mu hekalu, na wakachochea fujo. Kama kiongozi Muroma wa jeshi hangekuwa pale, Paulo angepigwa mupaka kifo. Kwa hiyo, ule kiongozi wa jeshi akaagiza Paulo afungwe. Kuanzia pale, kulipita zaidi ya miaka ine mbele Paulo akuwe tena huru. Lakini Paulo alikuwa angali mu hatari. Wakati ule kiongozi aliuliza Wayahudi juu ya nini walimushambulia Paulo, walimushitaki mambo mbalimbali. Juu watu wengi walikuwa wanalalamika wakati uleule, ule kiongozi hakuelewa kitu. Kisha, wale maaskari wakatosha Paulo pale. Wakati Paulo na maaskari wa Roma walikuwa karibu kuingia mu makao ya maaskari, Paulo aliambia hivi ule kiongozi: “Ninakuomba, uniruhusu niseme na watu hawa.” (Mdo. 21:39) Ule kiongozi alikubali, na Paulo akaanza kutetea imani yake kwa uhodari.

14, 15. (a) Paulo alifasiria Wayahudi nini? (b) Ule kiongozi wa jeshi alifanya nini ili ajue juu ya nini Wayahudi walimukasirikia sana Paulo?

14 Paulo alianza kwa kusema: ‘Musikilize namna ninajitetea.’ (Mdo. 22:1) Paulo alizungumuza na wale watu katika Kiebrania, na ile iliwatuliza. Aliwafasiria waziwazi juu ya nini alikuwa sasa mwanafunzi wa Yesu. Paulo alizungumuzia mambo fulani yenye Wayahudi wangechunguza na kuona kama ni ya kweli. Paulo alifundishwa na Gamalieli mwalimu mwenye kujulikana, na alitesa wanafunzi wa Yesu. Inawezekana watu fulani wenye walikuwa pale walijua ile mambo. Lakini, wakati alikuwa naenda Damasko, alipata maono kutoka kwa Yesu Kristo mwenye alikuwa amefufuliwa. Wale wenye walikuwa nasafiri pamoya na Paulo waliona mwangaza na walisikia sauti, lakini hawakuelewa maneno yenye ile sauti ilisema. Ile maono ilifanya Paulo akuwe kipofu. Kwa hiyo wenzake walimuongoza mupaka Damasko. Kule Anania, mwanaume mwenye Wayahudi wa ile eneo walijua, alifungua tena macho yake kwa muujiza.

15 Kisha Paulo akawaambia kama wakati alirudia Yerusalemu, Yesu alimutokea mu hekalu. Wakati Wayahudi walisikia vile, wakakasirika sana, na wakalalamika hivi: “Tosha mutu wa namna hiyo katika dunia, kwa maana hastahili kuishi!” (Mdo. 22:22) Ili kuokoa Paulo, ule kiongozi aliambia maaskari wake wamupeleke mu makao ya maaskari. Ule kiongozi alipenda sana kujua juu ya nini Wayahudi walimukasirikia sana Paulo. Kwa hiyo aliamuru maaskari wake wamupige na wamuulize maulizo. Lakini mbele wamupige, Paulo aliwaambia kama alikuwa raia wa Roma, na kulingana na sheria ya Waroma, hawakukuwa na haki ya kumupiga. Leo pia, waabudu wa Yehova wanatumia sheria mbalimbali ili kutetea imani yao. (Ona kisanduku “Sheria ya Roma na Raia wa Roma,” na “Kesi Mbalimbali za Wakati Wetu.”) Wakati ule kiongozi wa jeshi alisikia kama Paulo alikuwa raia wa Roma, alitambua kama alipaswa kutumia njia ingine ili apate habari zenye alikuwa natafuta. Siku yenye ilifuata, aliomba Sanhedrini (tribinali kubwa ya Wayahudi) ikutane. Na alimupeleka Paulo mbele ya ile tribinali.

KESI MBALIMBALI ZA WAKATI WETU

Kama Paulo, leo Mashahidi wa Yehova wanatumia sheria zenye kuwa mu maeneo yao ili kupigania uhuru wao wa kuhubiri. Wamekuwa na bidii katika “kutetea habari njema na kuifanya ikubaliwe kisheria.”​—Flp. 1:7.

Mu miaka ya 1920 na 1930, mamia ya Mashahidi wa Yehova walifungwa kwa sababu ya kugawia watu vichapo vyenye kutegemea Biblia. Kwa mufano kufikia mwaka wa 1926, kulikuwa kesi 897 zenye zilikuwa nachunga kusikilizwa ku tribinali za Alemanye. Kwa sababu ya zile kesi zote ndugu waliona kama ni jambo ya maana kuanzisha Idara ya Mambo ya Kisheria kwenye tawi ya Alemanye. Mu miaka ya 1930, katika inchi ya Amerika tu mamia ya Mashahidi wa Yehova walifungwa kila mwaka kwa sababu ya kuhubiri nyumba kwa nyumba. Mu mwaka wa 1936, hesabu ya Mashahidi wenye walifungwa ilifikia 1149. Ili kutolea ndugu muongozo wa kisheria, Idara ya Mambo ya Kisheria ilianzishwa mu Amerika. Kuanzia 1933 mupaka 1939, Mashahidi wa Yehova katika Romania walikuwa na kesi 530. Lakini wakati Mashahidi waliomba kusikilizwa na Tribinali Kubwa Zaidi ya Romania, walipata ushindi mara mingi. Ni vile mambo imekuwa mu inchi zingine za mingi.

Mashahidi wengine wameshitakiwa juu wamekatala kufanya mambo yenye kupingana na zamiri yao. (Isa. 2:2-4; Yoh. 17:14) Wapinzani wamewashitaki kwa uongo kama wanapinga serikali, na wakati fulani ile imefanya kazi yetu ikatazwe kabisa. Lakini kwa miaka mingi serikali za mingi zimetambua kama Mashahidi wa Yehova hawapinge serikali.g

g Ili kupata habari zaidi juu ya ushindi mbalimbali wenye Mashahidi wa Yehova wamepata mu inchi mbalimbali, ona sura ya 15 ya kitabu Ufalme wa Mungu Unatawala! na sura ya 30 ya kitabu Mashahidi wa Yehova​—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu.

“Mimi Ni Mufarisayo” (Mdo. 23:1-10)

16, 17. (a) Mambo ilikuwa namna gani wakati Paulo alizungumuza mbele ya Sanhedrini? Fasiria. (b) Paulo alionyesha namna gani kama iko munyenyekevu wakati alipigwa?

16 Paulo alianza kujitetea hivi mbele ya Sanhedrini: “Wanaume, ndugu, nimejiendesha kwa zamiri safi kabisa mbele ya Mungu mupaka leo.” (Mdo. 23:1) Mbele hata aseme jambo lingine, Biblia inasema hivi: “Halafu kuhani mukubwa Anania akaagiza wale wenye walikuwa wamesimama pembeni yake wamupige kwenye kinywa.” (Mdo. 23:2) Kufanya vile ilikuwa kumuzarau kabisa! Na kulionyesha kama kuhani mukubwa alikuwa na ubaguzi kwa sababu alimuhukumu Paulo kuwa muongo mbele hata ajitetee! Njo maana Paulo alisema hivi: “Mungu atakupiga, wewe ukuta wenye umepakwa rangi nyeupe. Je, unakaa ili kunihukumu kulingana na Sheria na wakati uleule unavunja Sheria hiyo kwa kuamuru nipigwe?”​—Mdo. 23:3.

17 Watu fulani walishangala sana, hapana juu ya mwenye alimupiga Paulo lakini juu ya maneno ya Paulo! Walimuuliza hivi: “Je, unatukana kuhani mukubwa wa Mungu?” Jibu ya Paulo ilionyesha kama alikuwa munyenyekevu na kama aliheshimia Sheria. Alisema hivi: “Ndugu, sikujua kama yeye ni kuhani mukubwa. Kwa maana imeandikwa, ‘Haupaswe kusema mubaya juu ya mutawala wa watu wako’”d (Mdo. 23:4, 5; Kut. 22:28) Sasa Paulo anaanza kufikiri nao mu njia ingine. Juu aliona kama Sanhedrini ilifanyizwa na Wafarisayo na Wasadukayo, alisema hivi: “Wanaume, ndugu, mimi ni Mufarisayo, mwana wa Wafarisayo. Ninahukumiwa kwa sababu ya tumaini la ufufuo wa wafu.”​—Mdo. 23:6.

Kiongozi wa dini iko naangalia kwa uangalifu andiko mu Biblia yake wakati ndugu iko namuhubiria.

Kama Paulo, wakati tunazungumuza na watu wa dini mbalimbali, tunatafuta jambo yenye tunakubaliana

18. Juu ya nini Paulo alijiita Mufarisayo, na namna gani tunaweza kutumia namna yake ya kufikiri na watu mu hali mbalimbali?

18 Juu ya nini Paulo alijiita Mufarisayo? Juu alikuwa “mwana wa Wafarisayo,” ni kusema watu wa familia yake walikuwa Wafarisayo. Kwa hiyo, wengi wangeendelea kumuona kuwa Mufarisayo.e Sasa, juu ya nini Paulo alijiita Mufarisayo hata kama Wafarisayo walikuwa naamini mambo ya uongo kuhusu ufufuo? Inasemekana kama, Wafarisayo waliamini kuwa wakati mutu anakufa, nafsi yake inaendelea kuishi na kama nafsi za watu wazuri zingeishi tena mu miili ya wanadamu. Paulo hakuamini ile mafundisho. Aliamini mambo yenye Yesu alifundisha juu ya ufufuo. (Yoh. 5:25-29) Lakini, Paulo alikubaliana na Wafarisayo kama kisha kifo kuko tumaini ya kuishi tena. Kwa upande mwingine, Wasadukayo hawakuamini kama kisha kifo kuko tumaini ya kuishi tena. Tunaweza pia kutumia ile namna ya kufikiri na watu wakati tuko nazungumuza na Wakatoliki ao Waprotestanti. Tunaweza kuwaambia kama, sawa wao siye pia tunaamini Mungu. Ni kweli kwamba pengine wanaamini Utatu, lakini siye tunaamini Mungu mwenye Biblia inazungumuzia. Hata vile, siye wote tunaamini kama kuko Mungu.

19. Juu ya nini mukutano wa Sanhedrini uligeuka na kuwa mabishano?

19 Maneno ya Paulo ilileta mugawanyiko katika Sanhedrini. Biblia inasema hivi: “Kukatokea muvurugo mukubwa, na wamoja kati ya waandishi wa chama cha Wafarisayo wakasimama na kuanza kubishana kwa ukali, na kusema: ‘Hatuone kosa lolote katika mutu huyu, lakini kama roho ao malaika alizungumuza naye​—.’” (Mdo. 23:9) Kusikia tu kama pengine malaika alizungumuza na Paulo, kulikwaza sana Wasadukayo, kwa sababu hawakuamini kama kuko Malaika! (Ona kisanduku “Wasadukayo na Wafarisayo.”) Mabishano ikakuwa nguvu sana mupaka ule kiongozi wa jeshi akaokoa tena Paulo. (Mdo. 23:10) Lakini, Paulo alikuwa tu angali mu hatari. Nini njo ingemufikia? Tutaona ile mu sura yenye kufuata.

WASADUKAYO NA WAFARISAYO

Sanhedrini yenye ilikuwa sawa vile serikali na tribinali kubwa ya Wayahudi ilifanyizwa na vikundi mbili vyenye kupingana, ni kusema Wasadukayo na Wafarisayo. Kulingana na mwanahistoria wa karne ya kwanza Flavius Josèphe, tofauti kubwa kati ya vile vikundi mbili ilikuwa kwamba Wafarisayo walilazimisha watu kufuata desturi za mingi. Kwa upande mwingine, Wasadukayo walifuata tu mambo yenye iliandikwa mu Sheria ya Musa. Lakini vile vikundi mbili viliungana ili kumupinga Yesu.

Inaonekana kuwa Wasadukayo wenye walifuata sana Sheria ya Musa, walikuwa na uvutano mukubwa kati ya makuhani, na Kuhani Mukubwa Anasi na Kayafa, wote walikuwa mu ile kikundi ya Wasadukayo yenye ilikuwa na uvutano mukubwa. (Mdo. 5:17) Lakini Josèphe anasema kama ni matajiri tu njo walikuwa “wanaamini mafundisho ya Wasadukayo.”

Kwa upande mwingine Wafarisayo walikuwa na uvutano kati ya watu wa kawaida. Lakini mawazo yao na desturi zao zilifanya watu waone kama ni muzigo kufuata Sheria. Tofauti na Wasadukayo, Wafarisayo waliamini kama mambo yote yenye inafikiaka mutu ilishapangwa mbele ya wakati. Waliamini kama nafsi inaendelea kuishi kisha mutu kufa. Na kisha inapata malipizi ao inapata zawabu kulingana na mambo yenye mutu alikuwa anafanya wakati alikuwa muzima.

a Juu kulikuwa Wakristo wengi Wayahudi, inawezekana makutaniko mingi ilikutana mu nyumba mbalimbali za ndugu.

b Miaka fulani kisha pale, mutume Paulo aliandika barua yake kwa Waebrania, na alionyesha wazi namna agano jipya ni ya hali ya juu sana kupita agano ya zamani, na kama agano jipya ilikamata nafasi ya agano ya zamani. Mafasirio yenye nguvu yenye alitoa ingesaidia Wakristo Wayahudi wajibie Wayahudi wenye walikuwa nazarau imani yao. Zaidi ya ile ilitia nguvu imani ya Wakristo fulani wenye walikuwa wangali wanakazia sana Sheria ya Musa.​—Ebr. 8:7-13.

c Watu wenye elimu wanasema kama wale wanaume walikuwa wamefanya naziri ya kuwa Wanaziri. (Hes. 6:1-21) Ni kweli kwamba naziri ya vile ilikuwa nafanywa chini ya Sheria ya Musa, na Sheria ya Musa haikukuwa natumika tena. Lakini, inawezekana Paulo aliona kama haikukuwa kosa wale wanaume watimize naziri yenye walimufanyia Yehova. Kwa hiyo, haingekuwa kosa kulipia mambo yote yenye walikuwa nayo lazima na kuwasindikiza. Hatujue ilikuwa naziri ya aina gani, lakini tunajua kama Paulo hangegaramia kutolewa kwa zabihu za wanyama (sawa vile Wanaziri walikuwa wanafanya) na kutumainia kama zile zabihu zingesafisha zambi ya wale wanaume. Kwa sababu Kristo alikuwa alishatoa zabihu kamilifu, zabihu za wanyama hazingeweza kufunika zambi. Ikuwe Paulo alifanya nini, tuko hakika kama Paulo hangekubali kufanya jambo yoyote yenye ingesumbua zamiri yake.

d Watu fulani wanasema kama Paulo alikuwa na matatizo ya macho na ile njo ilifanya asitambue kuhani mukubwa. Ao pengine juu hakukuwa Yerusalemu kwa muda murefu, hakujua ni nani njo alikuwa sasa kuhani mukubwa. Ao tena pengine hakuona muzuri ni nani aliagiza wamupige juu kulikuwa watu wengi.

e Mu mwaka wa 49 K.K.Y., wakati mitume na wazee walikusanyika ili kuzungumuzia ikiwa Watu wa Mataifa wanapaswa kufuata Sheria ya Musa, wamoja kati ya Wakristo wenye walikuwa pale waliitwa kuwa “wamoja kati ya wale wa zehebu la Wafarisayo wenye walikuwa wameamini.” (Mdo. 15:5) Ni wazi kama, wale waamini walikuwa wangali wanaitwa vile juu zamani walikuwa Wafarisayo.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine