Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • T-32 uku. 1-4
  • Ni nini inaweza kufanya familia ikuwe na furaha?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Ni nini inaweza kufanya familia ikuwe na furaha?
  • Ni Nini Inaweza Kufanya Familia Ikuwe na Furaha?
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Uko na Mawazo Gani Juu ya Wakati Wenye Kuja?
    Uko na Mawazo Gani Juu ya Wakati Wenye Kuja?
  • Kuko Siku Mateso Itaisha?
    Kuko Siku Mateso Itaisha?
  • Watu Wenye Wamekufa Wanaweza Kuishi Tena?
    Watu Wenye Wamekufa Wanaweza Kuishi Tena?
  • Uko na Mawazo Gani Juu ya Biblia?
    Uko na mawazo gani juu ya Biblia?
Ona Habari Zaidi
Ni Nini Inaweza Kufanya Familia Ikuwe na Furaha?
T-32 uku. 1-4

Ni nini inaweza kufanya familia ikuwe na furaha?

Unawaza ni . . .

  • upendo?

  • feza?

  • ao jambo lingine?

ONA JIBU LA BIBLIA

“Wenye furaha ni wale wenye wanasikia neno la Mungu na kulishika!”​—Luka 11:28, Tafsiri ya Ulimwengu Mupyra.

UTAPATA FAIDA GANI KAMA UNAAMINI JAMBO HILO?

Mutapendana sana mu familia.​—Waefeso 5:28, 29

Mutaheshimiana kabisa.​—Waefeso 5:33.

Mutakuwa na usalama kabisa.​—Marko 10:6-9.

Picha za familia yenye furaha: Mama na mutoto wake mwanamuke, bibi na bwana, wazazi pamoja na mutoto wao mwanaume

TUNAWEZA KUAMINI KABISA MAMBO YENYE BIBLIA INASEMA?

Ndiyo. Kuko sababu mbili hivi zenye kufanya tuamini mambo yenye Biblia inasema:

  • Mungu njo alianzisha familia. Biblia inasema kama “kila familia . . . inapata jina” kutoka kwa Yehova Mungu. (Waefeso 3:14, 15) Ni kusema, kama kuko familia, ni juu Yehova alianzisha familia. Juu ya nini ni muzuri kujua jambo hilo?

    Tukamate mufano: Kama unakula chakula kitamu chenye unafurahia, na unapenda kujua vitu vyenye walitia ndani, unaweza kuuliza nani? Kwa kweli, utauliza mutu mwenye alipika chakula hicho.

    Vilevile, kama tunapenda kujua mambo yenye kufanya familia ikuwe na furaha, ni muzuri tumuulize Yehova, juu yeye njo alianzisha familia.​—Mwanzo 2:18-24.

  • Mungu anakuhangaikia. Ni jambo la hekima familia zifuate mashauri yenye Yehova anatupatia kupitia Neno lake, Biblia. Sababu gani? “Kwa sababu yeye anawahangaikia ninyi.” (1 Petro 5:6, 7) Yehova anapenda mukuwe na maisha ya muzuri sana na mashauri yake inaletaka faida sikuzote!​—Mezali 3:5, 6; Isaya 48:17, 18.

FIKIRIA ULIZO HILI

Muzee wa kutaniko anashauria bibi na bwana wenye wangali vijana; wanasoma andiko la Biblia pamoja

Unaweza kufanya nini ili ukuwe bwana muzuri, bibi muzuri, ao muzazi muzuri?

Biblia inajibu ulizo hilo mu WAEFESO 5:1, 2 na WAKOLOSAI 3:18-21.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine