WIMBO 31
Utembee Pamoja na Mungu!
Maandishi
(Mika 6:8)
1. Utembee kwa kiasi
Pamoja na Yehova.
Tena ukuwe muaminifu,
Na umutegemee.
Na ukitii Neno yake
Hautaanguka.
Yeye atakuongoza
Ukimusikiliza.
2. Utembee kwa usafi
Pamoja na Yehova.
Hata upate jaribu gani
Atakusaidia.
Mambo ya kweli na ya haki,
na ya kusifiwa;
Uifikirie sana
Ili ubarikiwe.
3. Utembee kwa furaha
Pamoja na Yehova.
Umushukuru kwa wema wake
na kwa upendo wake.
Tembea pamoja na Mungu;
Imba kwa furaha.
Na watu wote wajue,
Kama ni Mungu wako.
(Ona pia Mwa. 5:24; 6:9; Flp. 4:8; 1 Ti. 6:6-8.)