Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 2/96 uku. 6
  • Kufundisha Neno La Mungu Kwa Kutumia Broshua

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Kufundisha Neno La Mungu Kwa Kutumia Broshua
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Tutangaze Habari Njema Ya Ufalme Kwa Msaada Wa Broshua
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Tutumie Broshua Mbalimbali Katika Mahubiri
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Tumwige Yehova Kwa Kuhangaikia Kwelikweli Wengine
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Unatumia Broshua Hizi?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2012
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1996
km 2/96 uku. 6

Kufundisha Neno La Mungu Kwa Kutumia Broshua

1 Watumishi wote wa Yehova waliojiweka wakf wanalo daraka la kufundisha jirani Neno la Mungu. Tunauona uzito wote wa daraka hilo tunapofikiria kwamba yeye ambaye alipewa mamlaka yote mbinguni na duniani anatukabizi bila shaka ujumbe wa kufanya ‘wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote, . . . tukiwafundisha.’ (Mat. 28:18-20) Basi mahubiri ya habari njema inadai kwamba tuwe wafundishaji.—2 Tim. 2:2.

 2 Katika Februari, tutatumikisha ufundi wetu mbalimbali wa wafundishaji ili kutolea watu broshua. Twaweza kutoa ndani yazo mawazo fulani ya kibiblia yenye kupendeza pia kutayarisha maelezo fulani yatakayotutolea nafasi ya kuanzisha mazungumzo.

 3 Ikiwa tunamtolea mtu broshua “Je! Mungu Anajali?” tunaweza kusema:

◼ “Tumewatembelea wengi wa majirani zako, na tumefikia kutambua kwamba wanahangaika sana wanapoona kuongezeka gafula kwa uvunjaji wa sheria, matisho ya ukatili na ujeuri. Kwa maoni yako, kwa nini mambo haya yanatendeka kwa kiwango kikubwa hivyo? [Acha mtu ajibu.] Ni jambo lenye kuvutia kuona kwamba Biblia imeyatangaza mambo hayo mapema. [Soma 2 Timotheo 3:1-3.] Tazama kwamba hayo yangepaswa kutokea katika ‘siku za mwisho.’ Jambo hilo linamaanisha kwamba kitu fulani kinafikia mwisho wacho. Unafikiri nini?” [Acha mtu ajibu.] Fungua broshua kwenye ukurasa 22, onyesha picha, pia chunguza andiko moja au mawili yanayotajwa kwenye ukurasa huo. Chukua mipango ya kurudia tena ili kumfasiria kwa nini sisi tunaamini kwamba baraka hizo zakaribia karibu.

 4 Labda tungependa kumtolea mtu broshua “Ni Nini Lililo Kusudi La Uhai? Wewe Waweza Kulipataje?” hivi:

◼ “Watu wengi wanaona vigumu kupata kusudi la maisha yao. Wachache tu ndio wenye furaha ya kadiri, lakini wengi zaidi wana maisha ya kuvunjika moyo na yenye mateso sana. Unafikiri kwamba ni maisha ya namna hayo ambayo Mungu alitazamia tuwe nayo? [Acha mtu ajibu.] Kulingana na Biblia, Mungu anapenda kwamba sisi tuishi katika ulimwengu kama huu.” Onyesha picha kwenye ukurasa 21, kisha kwenda kwenye kurasa 25 na 26, mafungu 4-6, na umfasirie kile Mungu ameahidi. Kwa kutayarisha ziara ifuatayo uliza hivi: “Namna gani tunaweza kuwa hakika kwamba Mungu atatimiza ahadi zake?”

 5 Tunaweza kumtolea mtu broshua “Kuishi Milele Duniani Katika Furaha!” kwa kuonyesha picha yote ya jalada na kumuuliza:

◼ “Je! ungependa kuishi katika ulimwengu kama huu wenye kujaa na watu wenye furaha? [Acha mtu ajibu.] Biblia yasema kwamba Mungu anapenda watu na anapenda kuwaona wakiishi milele duniani katika furaha.” Kwenda kwenye picha namba 49, na soma moja ya maandiko yanayotajwa. Kisha onyesha picha namba 50, na umfasirie mtu kile tunaweza kufanya ikiwa tunapenda kuishi katika Paradiso. Umtolee wazo la kurudia tena na kuzungumza naye juu ya ulazima wa kuwa na imani katika Yesu Kristo.

 6 Yehova ni mwenye furaha wakati sisi tunafanya ‘maendeleo yetu yaonekane kwa kujiangalia sana na fundisho letu.’ (1 Tim. 4:15, 16) Broshua zitakuwa zenye mafaa sana ili kusaidia wale ambao hutaka kusikia “habari njema ya maneno mazuri.”—Isaya 52:7.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine