Ziara Za Kurudia Zenye Matokeo Kwa Msaada Wa Fundisho Bora
1 Ziara za kurudia zinafanyiza sehemu ya maana na yenye furaha ya utumishi wetu. Kwa nini kurudia tena kwa bidii kukutana na watu walioonyesha kupendezwa? Kwa msaada wa kazi inayohusu kufanya wanafunzi, lile jina la Yehova lajulikana na kuheshimiwa, na wale wanaomhofu Mungu wanapokea msaada wanaouhitaji ili kuipata njia ya uhai. (2 Kor. 2:17 mpaka 3:3) Ikiwa tunafikia kufikiria kwamba kutakaswa kwa jina la Yehova kunahusika na kwamba uhai mwingi wa kibinadamu umo hatarini, tutasukumwa kujitayarisha vizuri kabla ya kurudia tena kuwaona watu.
2 Mfundishaji mzuri husaidia mwanafunzi kujenga juu ya msingi uliokwisha kuwekwa. Kama profesa anayeongezea siku kwa siku ujuzi wanaoupata wanafunzi, tunapaswa kuongeza mafasirio juu ya habari ileile tuliyozungumza tulipoonana mara ya kwanza. Jambo hilo lasaidia kulinda mfuatano wa wazo na kufuata mafikiri yenye kusonga mbele.
3 Ikiwa tunarudi kisha kumuachia mtu broshua “Je! Mungu Anajali?,” tunaweza kusema hivi:
◼ “Mara ya mwisho, tulizungumzia juu ya ‘siku za mwisho’ ambazo Biblia yasemea na kile jambo hilo lamaanisha kwetu. Bila shaka unajiuliza kile kinachotufanya tuhakikishe kwamba tunaishi katika siku za mwisho. (2 Tim. 3:1) Wanafunzi wa Yesu walikuwa na tamaa sana ya kupata jibu kwa ulizo hilo. [Soma Mathayo 24:3.] Katika jibu lake, Yesu alielezea hali ambazo tunaona zikituzunguka, kutia ndani taabu na ujeuri usiolinganishwa.” Onyesha wazi mambo yanayofanyiza ile ishara yanayopatikana katika mafungu 3 na 4, ukurasa 19. Ikiwa mtu anaitikia vizuri, mwonyeshe mambo mengine ya ile ishara yanayotajwa katika mafungu 5 mpaka 8, ukurasa 20. Tumuombe turudie tena ili kujibu maulizo yanayotokezwa kwenye ukurasa wa kwanza wa broshua.
4 Ili kudumisha kupendezwa ambako mtu aonyesha kutokana na broshua “Ni Nini Lililo Kusudi La Uhai? Wewe Waweza Kulipataje?” tungeweza kusema:
◼ “Nimefikiria sana kurudilia mazungumzo yetu kuhusu kusudi la uhai. Bila shaka unakubaliana na wazo kwamba Mungu alitaka kutuona sisi tukiishi katika furaha na amani duniani, na si katika misukosuko tunayoiona. Je! unawaza kwamba atatimiza ahadi yake?” [Acha mtu ajibu.] Soma Isaya 55:11, kisha uzungumze mawazo yaliyomo katika mafungu 25 mpaka 27, ukurasa 30. Tolea funzo la Biblia kama njia bora zaidi ya kufanya uhai wetu uwe na maana ya kwelikweli.
5 Ili kudumisha kupendezwa ambako mtu ameonyesha kutokana na broshua “Kuishi Milele Katika Furaha Duniani!” tunaweza kuionyesha tena na kusema hivi:
◼ “Tulizungumza kuhusu ulimwengu mzuri unaoonyeshwa kirangi juu ya jalada la broshua hii. Mimi nimekuja kukufasiria sababu gani ni jambo la lazima kwamba wale wanaotamani kuishi katika mahali hapa wawe na imani katika Yesu Kristo.” Onyesha picha 41 na usome Isaya 9:6. Kwa picha 62, usome Yohana 3:16 na kutia mkazo juu ya ulazima wa kutii. Fasiria kwamba Mashahidi wa Yehova wanasaidia watu; wanawafundisha namna gani kuzoea imani kwa kujifunza Biblia na kujitahidi kuyatumikisha mashauri yayo.
6 Tukague kila moja la ziara za kurudia zetu ili kuwe na matokeo mazuri. Ujiulize: Je! nilikuwa na jambo fulani la wazi akilini la kusema? Je! nilivutia uangalifu juu ya Biblia? Je! nilijenga juu ya misingi iliyowekwa wakati wa kukutana kwa mara ya kwanza? Je! utoaji wangu wa habari ulikuwa wenye kutengenezwa kwa kusudi la kuanzisha funzo la Biblia? Ikiwa tunaweza kujibu ndiyo kwa maulizo hayo, basi tunafanya yote tuwezayo ili kuwa wafundishaji wazuri wa lile Neno la Mungu.