Biblia: Kiongozi Kilichotolewa Na Mungu Kwa Watu Wote
1 Inakadiriwa kwamba Biblia bilioni nne zimechapwa katika lugha kubwa na ndogo zaidi ya 2,100, jambo linalowezesha Neno la Mungu lipatikane kwa zaidi ya asilimia 90 ya watu duniani. Hata hivyo, katika dunia kuna njaa “ya kusikia maneno ya Yehova.” (Amosi 8:11) Ni wengi walio na Biblia na ambao, ama hawaisomi, ama hawaielewi. Tunawezaje kuwasukuma waache Biblia iongoze kwa wazi maisha yao?
2 Katika Januari, tutatolea kitabu Biblia: Neno la Mungu au la Binadamu? Kwa wale watakaoonyesha kupendezwa, tutaweza kutoa pia tafsiri ya Biblia tunayofaidika nayo tangu sasa miaka 34: Tafsiri ya Ulimwengu Mpya. Kwa hiyo, tuonyeshe thamani ya usemi wake ulio rahisi na wa kisasa. Ikiwa, kwa shauku, tunasaidia wengine waone Biblia kuwa kiongozi kilichotolewa na Mungu kwa watu wote, tunaonyesha shukrani yetu yenye kina kirefu kuelekea zawadi hiyo ya Yehova.
3 Tunaweza kuanzisha mazungumzo kwa msaada wa trakti “Kwa Nini Kuitumaini Biblia,” kwa kusema kwa mfano:
◼ “Zaidi ya asilimia 90 ya watu duniani wanayo Biblia, lakini ingawa hivyo watu wachache tu ndio huisoma kikawaida. Je! unajua sababu?” Tusome mafungu mawili ya kwanza ya trakti na pia 2 Timotheo 3:16. Tupendekeze kitabu Neno la Mungu. Ikiwa kitabu kinakubaliwa, tujulishe bei. Ikiwa kitabu kinakataliwa, tuache trakti kwa mtu ili amalize kuisoma, tukivuta uangalifu wake kwenye kichwa kidogo, “Biblia inatabiri wakati ujao.”
4 Tunapokutana tena na wale waliokubali trakti “Kwa Nini Kuitumaini Biblia,” tunaweza kujaribu hivi:
◼ Baada ya kukumbusha mazungumzo yaliyotangulia, tusome mafungu mawili ya mwisho ya trakti. Tumuulize msikilizaji wetu ikiwa amekwisha kufikiri juu ya uwezekano wa kuishi milele duniani. Tusikilize jibu lake, kisha tuongeze: “Mashahidi wa Yehova wako hakika kwamba unabii wote wa Biblia utatimia, kutia ndani ule unaotangaza wakati ujao mzuri ajabu kwa wanadamu wanaokubaliwa na Mungu.” Tuonyeshe picha ya ukurasa 13 katika broshua Anataka. Ili kuanzisha funzo, tuende kwenye somo 5 na tupendekeze kuchunguza majibu kwa maswali yenye kuulizwa.
5 Katika maeneo ambamo watu wanashikamana na dini, tunaweza kujaribu kiingilio kifuatacho:
◼ “Tunatia moyo heshima kubwa zaidi kuelekea Biblia. Familia nyingi zina Biblia, lakini ni chache zinazoichunguza zinapopambana na matatizo makubwa. Je! wewe pia umeona hilo? [Tusikilize jibu.] Watu wanafikiri labda kwamba Biblia imekwisha kuzeeka. Kitabu hiki, Biblia: Neno la Mungu au la Binadamu? kinatoa uthibitisho wenye kusadikisha kwamba Biblia ni sahihi kisayansi na kwamba inatoa masuluhisho kwa matatizo makubwa tunayopambana nayo leo.” Tukazie mawazo fulani ya sura 8 au 12 ya kitabu, kisha tukitolee kwa msikilizaji wetu.
6 Tunaporudi kuona mtu tuliyeachia kitabu “Neno la Mungu,” tunaweza kusema:
◼ “Mara ya mwisho tuliona namna Biblia inavyotusaidia kusuluhisha matatizo magumu yanayojitokeza siku zetu. Inasaidia pia wale wanaoikubali kuwa Neno la Mungu kuishi maisha yenye furaha zaidi na yenye kutosheleza zaidi. Ningependa kukuonyesha moja ya kanuni za Biblia zenye kutenda kazi zinazoonyeshwa katika kitabu nilichokuachia.” Tuzungumzie kanuni ya kimaandiko inayoonyeshwa kwenye mafungu 3-6 ya sura 12, na tumalizie kwa kusoma fungu 7. Ikiwa mtu anaonyesha kupendezwa, tumtolee funzo kwa msingi wa kitabu Ujuzi au broshua Anataka.
7 Kichwa cha mazungumzo kifuatacho kinaweza kupendeza watu wazee-wazee:
◼ “Wakati fulani, Biblia ilikuwa ikisomwa katika nyumba zilizo nyingi na kanuni zayo ziliongoza maisha ya familia. Je! ilikuwa ikifanyika hivyo mahali penu? [Tusikilize jibu.] Leo, yaelekea kwamba watu wengi ni wenye shughuli sana ili kuweza kusoma Biblia, au labda wanafikiri kwamba kanuni za kiadili za Biblia hazitendi tena kazi leo. Sura 13 ya kitabu hiki Biblia: Neno la Mungu au la Binadamu? inasimulia kisa cha watu watatu ambao, baada ya kujifunza Biblia, waliweza kubadili maisha yao. Ikiwa unapenda kusoma namna uwezo wa Neno la Mungu ulivyowasaidia, nitakuwa mwenye furaha kukuachia kitabu hiki.”
8 Wakati wa ziara yetu ya pili, tunaweza kusema:
◼ “Wakati wa mwisho, tulikubaliana kusema kwamba kanuni za kiadili za Biblia zinazarauliwa na jamii ya sasa. Kwa maoni yako, je! tunapaswa kujisikia wenye kuhusika? [Tusikilize jibu.] Yesu Kristo alifasiria kwamba kutwaa ujuzi juu ya Mungu kuna thamani kubwa.” Tusome Yohana 17:3. Kisha tufungue kitabu Ujuzi kwenye sura 1 na tuzungumzie fungu 5. Tuseme juu ya programu yetu ya funzo la Biblia bila malipo na tupendekeze kumuonyesha jinsi funzo linavyoendeshwa.
9 Tuombe Yehova abariki jitihada zetu zote za kuelekeza uangalifu wa watu kwenye Biblia, kiongozi alichotoa kwa watu wote!