Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 1/98 uku. 3-4
  • Tungepaswa Kuwa Walimu, Si Wahubiri Tu

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Tungepaswa Kuwa Walimu, Si Wahubiri Tu
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Jinsi Ya Kufanya Wanafunzi Kwa Msaada Wa Kitabu Ujuzi
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Tazamo Linalosonga Mbele Juu Ya Kazi Ya Haraka Ya Kufanya Wanafunzi
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Mafunzo Ya Biblia Zaidi Yanatakwa
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Unaweza Kusaidia mu Kazi ya Kufanya Wanafunzi?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2021
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1998
km 1/98 uku. 3-4

Tungepaswa Kuwa Walimu, Si Wahubiri Tu

1 Mtu fulani alisema kwamba “Mashahidi wa Yehova wamejaza kihalisi dunia na ushahidi wao.” Hilo liliwezekanaje? Kazi hii ya ushahidi haikufanyika kwa uwezo wa mwanadamu, lakini kupitia utendaji wa roho ya Mungu juu ya watumishi wake kwa kadiri wanavyofaidika na mipango mbalimbali inayochukuliwa ili kutimiza utume wao wa kuhubiri na kufundisha.​—Zek. 4:6; Mdo. 1:8.

2 Ukurasa uliochapwa ni njia moja yenye matokeo ya kutimiza kazi yetu ya kuhubiri. Muda wa miaka mingi, Mashahidi wa Yehova walichapa na kugawa mabilioni ya vitabu, broshua, magazeti na trakti ili kujulisha habari njema za Ufalme. Ripoti zilizotolewa katika Kitabu-Mwaka 1997 zinaonyesha kwamba uchapaji wa vichapo umefikia viwango vya juu. Kwa siku ya leo, zaidi ya milioni  91 ya nakala za Tafsiri ya Ulimwengu Mpya zimechapwa. Kwa kipindi cha mwaka mmoja, uchapaji wa Mnara wa Mlinzi na Amkeni katika United States (Amerika) uliongezeka kwa asilimia 7.1. Katika Ujerumani, uliongezeka kwa asalimia 35. Zaidi ya theluji (nusu ya tatu) moja ya magazeti ambayo tawi la nchi hiyo lilichapa yalikuwa ya kutumwa Urusi.

3 Kwa nini kuna uhitaji kama huo wa vichapo? Ulimwenguni pote, mwaliko wa kutoa ushahidi mahali pote watu wanapopatikana uliamsha itikio la ajabu. Wengi wetu wanapanua utendaji wao kwa kuhubiri katika nafasi za watu wengi, katika barabara na katika mitaa ya kibiashara, jambo ambalo linakuwa na matokeo ya kuongeza hesabu ya vichapo vinavyoachwa kwa watu wanaoonyesha kupendezwa. Wengi kati yao walipata mara haba, au hata hawakupata kamwe, nafasi ya kusikia ujumbe wa Ufalme. Ili kutosheleza uhitaji huo, makutaniko yana rundo ya vichapo vinavyotumiwa kwenye aina mbalimbali ya huduma.

4 Tuna Kusudi Gani Tunapogawa Vichapo? Kusudi letu si kugawa vichapo tu. Utume wa kufanya wanafunzi ni wenye sehemu mbili: kuhubiri na kufundisha. Kwanza, tuna pendeleo la kuhubiri habari njema ya Ufalme, yaani kuonyesha watu kwamba Ufalme ndilo tumaini pekee kwa wanadamu. (Mt. 10:7; 24:14) Vichapo vyetu vyenye kutegemea Biblia ni njia iliyojaribiwa na yenye matokeo ili kuamsha kupendezwa kwa ajili ya Ufalme na kutoa ujuzi juu ya huo.

5 Pili, ikiwa tunataka kufanya wanafunzi, tunapaswa kufundisha maneno yote Yesu aliyoamuru. (Mt. 11:1; 28:19, 20) Hapo tena, vichapo hutimiza daraka la maana katika jitihada zetu za kuingiza ukweli katika moyo wa wanafunzi, tukiwasaidia kuwa wafuasi.

6 Labda watu wanaokubali vichapo ni ‘wasikiaji wa neno’, lakini kuna uhakika mdogo kwamba wawe watendaji ikiwa hawashughulikiwi. (Yak. 1:22-25) Wachache wao ndio watakuwa wanafunzi ikiwa hakuna mtu wa kuwaongoza. (Mdo. 8:30, 31) Wanahitaji msaada wa mwalimu ili wasadikishwe na ukweli ulio katika Maandiko. (Mdo. 17:2, 3) Kusudi letu ni kuwaongoza wafanye maendeleo hadi kujitoa wakfu kwa Mungu na kubatizwa, na pia kuwatolea mazoezi yatakayowafanya wawe wenye kufaa kufundisha wengine.​—2 Tim. 2:2.

7 Ni Jambo la Maana Sana Kwamba Kuwe Walimu Wengi Zaidi: Tunapohubiri, tunatangaza peupe habari njema. Hata hivyo, kufundisha mtu mwingine ni kumtolea elimu ya hatua kwa hatua. Huku mahubiri yakiwa yanamjulisha jirani yetu ujumbe wa Ufalme, ufundishaji unamsaidia kukubali habari njema na unamsukuma kutenda. (Luk. 8:15) Mwalimu anafanya mengi zaidi ya kutangaza: anafasiria, anatoa sababu kwa msingi wa maelezo yenye kushikamana, anatoa uthibitisho na anajionyesha mwenye kusadikisha.

8 Hesabu kubwa zaidi iwezekanavyo kati yetu wangepaswa kuwa waalimu, si wahubiri tu. (Ebr. 5:12a) Ugawaji wa vichapo ni sehemu ya maana sana ya kazi yetu, lakini fanikio katika utimizo wa kusudi la pili la huduma yetu hutegemea, kwa vyovyote, yale tunayofanya kwa kufundisha. Ingawa tunaweza kufurahia kugawa vichapo, ikiwa tunataka kutimiza kikamili huduma yetu, hatupaswi kuona hilo kuwa kusudi letu la kwanza. (2 Tim. 4:5) Vichapo tunavyoacha vinafungua kwa matokeo njia kwa uwezekano mbalimbali wa kufundisha jirani yetu ukweli.

9 Tufanye Ziara za Kurudia kwa Ajili ya Kuanzisha Mafunzo ya Biblia: Ni kweli kwamba kila mmoja wetu amekwisha kuacha hesabu fulani ya vitabu, broshua na magazeti, jambo lililotokeza orodha ya ziara za kurudia. Tungepaswa kuweka kando wakati kikawaida ili kukomaza kupendezwa. Tunaporudi kuona watu, kusudi letu la kwanza si kuwaachia vichapo vingine tu, lakini kuwatia moyo wasome vile walivyo navyo tayari na kufaidika navyo. Sisi wenyewe tungeweza kufanya maendeleo kwa kadiri gani ikiwa mtu fulani hangekuja kutuona mara nyingi ili kutusaidia kutwaa ujuzi sahihi?​—Yohana 17:3.

10 Tufanye kupendezwa kokote kuzae matunda tukiwa na kusudi la kuanzisha funzo la Biblia, iwe kwa msingi wa broshua Mungu Anataka Nini Kwetu au kitabu Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele. Vichapo hivyo viwili vinatoa ujumbe wa Ufalme kwa njia yenye kusikika kwa urahisi. Broshua Anataka ina funzo kamili la Biblia linalozungumzia mafundisho ya msingi ya Biblia. Kitabu Ujuzi kinawezesha kufundisha ukweli kwa undani, lakini kwa urahisi, uelewevu na kwa maneno machache.

11 Kama inavyofasiria nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Julai 1996, programu iliyorekebishwa ya mafundisho inarahisisha kazi kwa mwalimu na kwa mwanafunzi. Tuchunge nakala moja ya nyongeza hiyo karibu ili kurudilia njia na ufundi wa kufundisha uliyoonekana kuwa wenye matokeo. Madokezo fulani yanaonyesha namna ya kumuonyesha mwanafunzi kupendezwa kwa kwelikweli, kiasi cha mawazo ya kuzungumzia muda wa kila funzo, namna ya kujibu maswali yasiyohusiana moja kwa moja na kichwa cha habari, namna mwalimu na mwanafunzi wanapaswa kujitayarisha kimbele na namna ya kuongoza mwanafunzi kwenye tengenezo la Yehova. Kwa kutumikisha madokezo hayo, wengi wetu, kutia ndani wapya, tutaweza kuongoza mafunzo yenye kufanya maendeleo.

12 Ripoti Fulani Zinazoonyesha Matokeo Mazuri Yaliyopatikana: Broshua Anataka na kitabu Ujuzi vinaonekana kuwa msaada mkubwa katika kufanya wanafunzi kwa uharaka zaidi. Tangu alipopata broshua Anataka, ndugu anayeishi Bolivia aliitumia ili kuanzisha funzo na mwanamume mmoja. Miezi minne baadaye, wakati wa kusanyiko la wilaya, mwanamume huyo alikuwa miongoni mwa kikundi chenye furaha cha waliokuwa tayari kupokea ubatizo!

13 Wanapofika mwishoni mwa uchunguzi wa kitabu Ujuzi, wengi hujisikia wenye kusukumwa kutoa maisha yao wakfu kwa Yehova. Katika Angola, hesabu ya mafunzo ya Biblia yaliyoongozwa na wahubiri wa kutaniko moja iliongezeka toka 190 hadi 260, huku hudhurio kwenye mikutano likiongezeka mara mbili, kutoka wahudhuriaji 180 hadi 360, miezi minne tu baada ya kitabu Ujuzi kuanza kutumiwa katika eneo. Punde si punde, lilionekana kuwa jambo la lazima kuunda kutaniko jipya.

14 Baada ya kuanzisha funzo la kwanza na kitabu Ujuzi, ndugu mmoja alisema kwamba hilo lilikuwa “rahisi ikiwa yule anayeongoza funzo anatosheka na kuuliza maswali, kusoma maandiko fulani yenye kufaa na ikiwa anahakikisha kwamba mtu amesikia.” Alikuwa akifikiri sikuzote kwamba ni wahubiri wenye ujuzi sana ndio peke yao waliokuwa na uwezo wa kuongoza mafunzo ya Biblia yenye kuendelea na kwamba yeye mwenyewe hangeweza hilo kamwe, lakini alitambua kwamba alikuwa na uwezo huo na akasema: “Ikiwa ninaweza kufanya hilo, basi kila mtu anaweza.”

15 Ni kwa kuongoza mafunzo ya Biblia, yaliyo sehemu ya huduma yetu, kwamba tunafikia kusudi letu la kufanya wanafunzi. Wale wanaokomaza uwezo wao wa akili katika upande huo wa huduma yetu watavuna kutosheka kwa kweli na faida nyingi. Na isemwe juu yetu pia kwamba ‘tunahubiri Ufalme wa Mungu kwa uhuru wa usemi ulio mkubwa zaidi sana’!​—Mdo. 28:31.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine