Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 2/98 uku. 6
  • Tufurahie Kutoa Ushahidi Kamili

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Tufurahie Kutoa Ushahidi Kamili
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Utoaji Mbalimbali Uliopendekezwa kwa Ajili ya Utumishi wa Shambani
    Huduma Yetu ya Ufalme—2005
  • Ujuzi Utokao Kwa Mungu Unajibu Kwa Maulizo Mengi
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Utoaji Uliopendekezwa kwa Ajili ya Utumishi wa Shambani
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Tutoe Habari Njema, Tukitambua Kwamba Wakati Unasonga Mbele
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1998
km 2/98 uku. 6

Tufurahie Kutoa Ushahidi Kamili

1 Kila mmoja wetu anapenda kufanya mambo anayojua kufanya vizuri. Kulingana na Marko 7:37, makutano yalikuwa yakisema juu ya Yesu: “Amefanya mambo yote vema.” Si jambo la kustaajabisha, basi, kwamba Yesu alifurahia kufanya mapenzi ya Yehova! (Ona Zaburi 40:8.) Kwa kufikiri vema juu ya madokezo yatakayofuata, tutapata sisi pia furaha kutii amri ya Yesu, yaani kuhubiri watu na kutoa ushahidi kamili. (Mdo. 10:42) Mnamo Februari, tutatolea ama kitabu chenye kurasa 192 kilichotangazwa kabla ya 1985, ikiwa kutaniko linacho katika stoki, ama kitabu Kuishi Milele. Tunawezaje kutoa ushahidi kamili kwa msaada wa vichapo hivyo?

2 Kwa kuwa watu wengi ni wenye kushughulikia afya yao, tungeweza kusema:

◼ “Ingawa maendeleo makubwa ya utibabu, ugonjwa bado unatokeza mateso mengi. Kwa maoni yako, tunawezaje kufasiria hilo? [Tusikilize jibu.] Yesu alisema kwamba tauni, magonjwa ya kuambukiza, yangekuwa ishara ya siku za mwisho. (Lk. 21:11) Lakini Biblia inasema pia juu ya wakati ambapo ugonjwa utatoweka. [Tusome Isaya 33:24.] Ona sababu za kutumaini katika fundisho hilo la msingi la Biblia ambazo kitabu hiki kinatutolea.” Tutaje mawazo fulani yenye kufaa kutokana na kitabu tunachoonyesha, kisha tukitolee msikilizaji wetu, na hilo kwa mchango wa sasa.

 3 Tunapohubiri kwa namna ya vivi hivi kando kando ya maduka, tungeweza kumsalimu mtu na kumuuliza:

◼ “Je! hauoni kwamba maisha yanakuwa magumu sana leo hivi kwamba inakuwa vigumu zaidi na zaidi kupata chakula hadi mwisho wa mwezi? [Tusikilize jibu.] Je! unafikiri kwamba siku fulani tutakuwa na usalama wa kweli wa vitu vya kimwili?” Tusikilize jubu. Kisha tutaje andiko la Biblia lenye kufaa kutokana na kitabu tunachoonyesha. Tuendelee: “Kitabu hiki kinafasiria namna gani, kupitia Ufalme wake, Mungu atasuluhisha matatizo yanayofanya maisha kuwa magumu sana leo.” Tutolee kitabu. Kisha tungeweza kumwambia namna tulivyofurahia mazungumzo, na kumuuliza: “Je! ingewezekana kuendeleza mazungumzo haya siku nyingine?” Kwa njia hiyo, tutapata labda anwani ya mtu.

 4 Ikiwa tunatumia kitabu “Kuishi Milele,” tutakuwa labda na nafasi ya kujaribu utangulizi ufuatao juu ya amani ulimwenguni:

◼ “Kwa maoni yako, kwa nini ni jambo ngumu kusimamisha amani ulimwenguni? [Tusikilize jibu, kisha tuonyeshe picha ya kurasa 20-1.] Picha hii inaonyesha tukio la kibiblia linaloelezwa katika kitabu cha Ufunuo. [Tusome Ufunuo 12:​7-9, 12 katika fungu 17. Kisha tusome maneno yaliyo chini ya picha.] Basi, Ibilisi alitupwa duniani, na moja ya matokeo ya tukio hilo ni kuondolewa kwa amani ulimwenguni. Kitabu hiki kinajibu maswali mengi ya lazima. Ningefurahi kukuachia chenyewe ikiwa unatamani kukisoma.” ​— Kwa ajili ya utoaji mwingine wenye matokeo wa kitabu Kuishi Milele tuchunguze upya ukurasa wa mwisho wa chapa za Huduma Yetu ya Ufalme za Machi 1995, Machi 1994 na Januari 1993.

 5 Tunaporudi tena kuona wale walioonyesha kupendezwa, tunaweza kujaribu kuanzisha funzo la Biblia kwa kutumia utangulizi ufuatao:

◼ “Wakati wa mazungumzo yetu ya kwanza, ulitoa wazo lenye kupendeza sana. [Tutaje wazo moja alilosema msikilizaji wetu.] Nilifikiri juu ya hilo, na ningependa kukuonyesha yale niliyopata kwa kufanya utafiti fulani. [Tuchunguze pamoja na mtu andiko la Biblia lenye kufaa.] Tunatolea funzo pasipo malipo, ambalo limekwisha kusaidia mamilioni ya watu kuchimba kwa undani mafundisho ya msingi ya Biblia kwa kipindi kidogo cha wakati. Uchunguzi huo wa Biblia unaweza kukutolea tumaini katika utimizo usiokosea wa ahadi za Mungu.” Tutaje maswali fulani ambayo funzo litajibu. Ikiwa mtu anakataa toleo letu, tumfasirie kwamba tunatoa pia funzo la pekee la mfululizo, linaloomba tu dakika 15 kila juma kwa muda wa majuma 16. Tumuonyeshe broshua Anataka, tuifungue kwenye somo 1 na tuulize msikilizaji wetu ikiwa tunaweza kumfasiria, kupitia somo hilo, namna funzo linavyoendeshwa.

 6 Ikiwa tunatimiza kazi yetu kwa ufundi, tutapatia ndani furaha. ‘Tukaze uangalifu daima’ kwa kutoa ushahidi kamili, na tuwe wenye furaha kutimiza vema aina zote za huduma yetu.​—1 Tim. 4:16.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine