Tualike Yeyote Aliye Na Kiu
1 Kama alivyotabiri Amosi, jamii ya kibanadamu inakabiliwa leo na “kiu, si kiu cha maji, lakini cha kusikia neno la Yehova.” (Amosi 8:11) Ili kusaidia wale wanaoteswa na ukame huo wa kiroho, tunajulisha mipango ambayo Mungu alichukua ili kukomboa wanadamu watiifu kutoka dhambi na kifo, mipango inayoonyeshwa katika kitabu cha mwisho cha Ufunuo kwa mfano wa “mto wa maji ya uhai.” Tunalo pendeleo la kualika yeyote aliye na kiu cha haki ‘achukue maji ya uhai bure.’ (Ufu. 22:1, 17) Tutafanyaje hilo mnamo Machi? Kwa kutolea wale wanaoonyesha kupendezwa kwenye unyofu kitabu Ufunuo: Upeo Wao Mtukufu U Karibu! Labda tungetaka kujaribu matangulizi yafuatayo.
2 Watu wengi wanapendezwa na maswali ya afya; hivyo tutaona labda utangulizi huu kuwa wenye kupendeza:
◼ “Watu wengi wanahangaika juu ya bei inayopanda zaidi na zaidi ya matunzo ya kitiba ya hali ya juu. Je! umekwisha kufikiri juu ya hilo? [Tuacha mtu ajibu.] Je! unaona suluhisho la mwisho kwa tatizo hilo? [Tuacha mtu ajibu.] Ona tazamio la ajabu.” Tusome Ufunuo 22:1, 2. Tufungue baadaye kitabu Upeo wa Ufunuo kwenye picha ya kurasa 308-9 na tutoe maelezo juu ya picha kwa msingi wa fungu 22 la ukurasa 311. Tumalizie kwa kusema: “Kitabu hiki kinafasiria Ufunuo mstari kwa mstari.” Ikiwa msikilizaji wetu anaonyesha kupendezwa kwa kweli, tumtolee kitabu kwa bei ya sasa. Tuchukue mipango ili kuonana naye tena.
3 Tutakapofanya ziara ya kurudia, tungeweza kukumbusha mazungumzo yetu yaliyotangulia kwa kusema hivi:
◼ “Wakati wa mazungumzo yetu ya nyuma, tulisema juu ya suluhisho la mwisho kwa matatizo ya afya. Je! unafikiri kwamba siku moja hakuna mtu atakayekuwa mgonjwa tena? [Tuache mtu ajibu.] Angalia maneno haya yenye kustaajabisha.” Tusome Isaya 33:24. Kisha tufungue broshua Anataka kwenye somo 5, tuchunguze mafungu 5 na 6 kwa kuuliza maswali yenye kuambatana nayo mwanzoni mwa somo na kwa kuchukua mojawapo ya maandiko ya Biblia yanayotajwa. Tufasirie kwamba kutoweka kwa ugonjwa na kifo ni katika utimizo wa kusudi la kwanza la Mungu kuhusu dunia. Tupatane ili kuzungumzia mafungu 1 hadi 4 na 7 ya somo lilelile.
4 Ikiwa habari za karibuni zilionyesha kifo cha ghafula cha mtu fulani, tungeweza kujaribu njia hii:
◼ “Bila shaka umesikia wakisema juu ya [taja habari]. Wakati uhai unapotoweka kwa ghafula katika msiba, watu wengi wanajiuliza ni kitulizo gani cha kutolea jamaa za waliopatwa na msiba. Wewe unafikiri nini?” Tuache mtu ajibu. Tufungue kitabu Upeo wa Ufunuo kwenye ukurasa 299 ne tuonyeshe picha ya ufufuo. Tuendelee kwa kusema: “Watu wengi wanashangaa wanaposikia kwamba wenye haki na wasio haki watarudishwa tena kwenye uhai katika Paradiso duniani. [Tusome Matendo 24:15, linalotajwa kwenye fungu 9, ukurasa 297, na tutoe mafasirio yanayoonyeshwa kwenye fungu 10.] Kitabu hiki kinaonyesha habari nyingine nyingi juu ya kusudi la Mungu kuhusu wakati ujao. Ikiwa unataka kujua mengi zaidi juu ya jambo hilo, ninaweza kukuachia nakala hii.” Tupendekeze kurudi na tuandike mambo yanayompendeza na mahangaiko ya msikilizaji wetu.
5 Wakati wa ziara ya kurudia, tuambatanishe utoaji wetu na mtu. Labda tungeweza kutoa maelezo ya aina hii:
◼ “Mara ya mwisho tulipoongea, ulisema jambo fulani lililonipendeza juu ya kusudi la Mungu kuhusu dunia. [Tukumbushe yale mtu yule aliyosema.] Nimepata mawazo ambayo, kwa maoni yangu, yatakupendeza.” Tufungue broshua Anataka kwenye somo 5. Tusome mafungu yote yanayovutia uangalifu wa mtu na tuyazungumzie. Baada ya kupatana kwa ajili ya kuendeleza uchunguzi wa somo, tuache aliko (ikiwa linapatikana) linaloonyesha saa ya mikutano ya kutaniko. Tufasirie ni nini hotuba ya peupe na tualike mtu kuihudhuria.
6 Ikiwa tunapendelea utoaji wenye kurahisishwa kwa msaada wa trakti, tunaweza kujaribu hili:
◼ “Ningependa kukuachia trakti hii yenye kichwa Kuna Tumaini Gani Kwa Wapendwa Waliokufa?” Tuitolee mtu na tumwalike kufuata usomaji wa fungu la kwanza. Tumwache ajibu kwa ulizo linalotokezwa na sentensi ya mwisho. Tusome fungu la pili, kisha tuonyeshe picha ya ukurasa 299 ya kitabu Upeo wa ufunuo. Tuendelee kwa kusema: “Kitabu hiki kinafasiria zaidi kwa urefu ufufuo na ahadi nyingine za ajabu za Biblia kwa ajili ya wakati ujao. Ikiwa unataka kukisoma, basi hiki ni chako.” Tujulishe bei, kulingana na bei ya sasa, na tuchukue mipango kwa ajili ya ziara ya kurudia.
7 Mwaliko wenye kusihi tunaotolea wanadamu wenzetu unaweza kuwavuta kwenye maji ya uhai ambayo Yehova anamwanga kwa sasa. Kwa sababu hiyo, kwa yeyote aliye na kiu tuseme: “Njoo!”—Ufu. 22:17.