‘Wenye Kuandaliwa Vifaa Kikamili Kwa Ajili Ya Kila Kazi Njema’
1 Watu wa Yehova leo hufaidika na chakula cha kiroho kizuri na kingi. (Is. 25:6) Tuna furiko la habari za kibiblia za kuchunguza wakati wa funzo la kibinafsi au la jamaa, wakati wa mikutano ya kutaniko au makusanyiko. Lakini, je! tunafaidika kikamili na hilo tukiwa na kusudi la ‘kuwa hodari, walioandaliwa vifaa kikamili kwa ajili ya kila kazi njema’?—2 Tim. 3:17.
2 Tufikiri kidogo juu ya orodha ya vyakula vya kiroho vya mwaka 1998, ambao nusu yake imekwisha kupita! Wakati wa mikutano ya kutaniko ya kila juma, tunavumbua hatua kwa hatua nukta kuu za vitabu 23 vya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo, tunatafakari juu ya maisha ya watu 49 wa kibiblia kwa msaada wa habari zinazotolewa na kitabu Auxiliaire pour une meilleure intelligence de la Bible na tunachunguza kurasa 138 za kitabu Wapiga-Mbiu. Tunajifunza pia sehemu ya tatu ya kitabu Ujuzi, karibu kitabu Furaha ya Familia chote, na pia kitabu Neno la Mungu chote. Kwa kuongezea, chapa 12 za Huduma Yetu ya Ufalme, makala 52 za Mnara wa Mlinzi na karibu hesabu iyo hiyo ya hotuba za watu wote zinazozungumzia habari mbalimbali za kibiblia vinatulisha. Programu zenye kuandaliwa na makusanyiko huongezwa kwa hayo yote. Ni utajiri wa kiroho kama nini unaotolewa kwetu!
3 Tuwe Wenye Shukrani kwa Mipango Anayoichukua Yehova: Ili kufaidika kikamili na hiyo, tunapaswa kufahamu kwa nini Yehova anatutolea furiko hilo. Kwa kujilisha kutokana na vitu hivyo vizuri, tunajenga imani yetu na kutia nguvu vifungo vyetu pamoja naye. (1 Tim. 4:6) Hata hivyo, chakula cha kiroho hakitolewi kwetu kwa ajili ya kufunzwa kwetu peke yake. Kinatusukuma kujulisha kweli kwa wengine na kinatutolea vifaa ili kutufanya kuwa wahudumu wenye matokeo wa habari njema.—2 Tim. 4:5.
4 Tusidharau kamwe mahitaji yetu ya kiroho, lakini tuwe sikuzote na tamaa kubwa kwa ajili ya mipango mingi ya kiroho inayotokana na meza ya Yehova na ambayo hutokeza furaha. (Mt. 5:3; 1 Pet. 2:2) Ili kufaidika nayo kikamili, ni jambo la lazima kutoa wakati wa kutosha na kwa ukawaida kwa ajili ya usomaji wa Biblia, kibinafsi na katika familia, pia kwa ajili ya kuhudhuria mikutano. (Efe. 5:15, 16) Baraka zinazotokana na hilo zitapatana na kitia-moyo chenye kupuliziwa ambacho Paulo alitoa kwa Wakristo Waebrania waaminifu kwenye Waebrania 13:20, 21.