Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 8/98 uku. 8
  • Wanadamu Wenzetu Wanahitaji Kusikia Habari Njema

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Wanadamu Wenzetu Wanahitaji Kusikia Habari Njema
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Tutumie Broshua Mbalimbali Katika Mahubiri
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Tuhubirie “Watu wa Namna Zote”
    Huduma Yetu ya Ufalme—2012
  • Tutangaze Habari Njema Ya Ufalme Kwa Msaada Wa Broshua
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Kufundisha Neno La Mungu Kwa Kutumia Broshua
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1998
km 8/98 uku. 8

Wanadamu Wenzetu Wanahitaji Kusikia Habari Njema

1 Mungu anapenda “kwamba watu wa namna zote waokolewe na kuja kwenye ujuzi sahihi wa kweli.” (1 Tim. 2:4) “Watu wa namna zote” humaanisha wanadamu wenzetu wote. Ili habari njema iwaguse, acheni tubadili utoaji wetu mbalimbali na tufikiri juu ya kile kiwezacho kupendeza kila mmoja wao. (1 Kor. 9:19-23) Tengenezo la Yehova linatuandalia vifaa vitakavyotusaidia kugusa moyo wa wale walio “na mwelekeo ufaao kwa ajili ya uhai udumuo milele.” (Mdo. 13:48) Acheni tuone namna ya kutumia broshua mbalimbali, tutakazotolea mnamo Agosti na Septemba, ili kutimiza mahitaji ya kiroho ya jirani yetu.

2 Broshua Tunazotolea: Madokezo yafuatayo yataweza kuwa yenye mafaa kwetu ili kutolea broshua fulani fulani. Kila dokezo hutia ndani: (1) ulizo moja linalochochea kufikiri ili kuanzisha mazungumzo, (2) rejezo kwenye broshua ambayo ndani yake tutapata nukta za mazungumzo na (3) andiko la Biblia lenye kufaa ambalo tutaweza kusoma wakati wa mazungumzo. Kuhusu sehemu yenye kubaki ya utoaji, tutumie maneno yetu wenyewe na tuangalie (to take into consideration) kupendezwa kwa msikilizaji wetu. Utoaji wenye habari zote wa broshua nyingi unapatikana katika chapa iliyotangulia ya Huduma Yetu ya Ufalme iliyotajwa.

Je! Kweli Mungu Anatujali?

Kwa maoni yako, kuna tumaini gani kwa wale wanaoteswa?​—Kurasa 27-8, mafungu 23-7; Isa. 65:17, 18; km-SW 8/97 ukurasa 8.

Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai​—Wewe Waweza Kulipataje?

Inawezekanaje kwamba watu wengi leo hawatosheki na hali yao?​—Kurasa 29-30, mafungu 2, 25-6(à vérifier); Zab. 145:16; km-SW 8/96 ukurasa 8.

Kuishi Milele Duniani Katika Furaha!

Je! umekwisha kujiuliza kile ambacho Yesu Kristo hufanya kwa sasa?​—Picha 41-2; Ufu. 11:15; km-SW 9/96 ukurasa 4.

Serikali Itakayoleta Paradiso.

Je! ungependa kujua ni Ufalme gani ambao kwa ajili ya huo Yesu alifundisha kuomba?​—Ukurasa 3; Mt. 6:9, 10; km-SW 9/96 ukurasa 4.

Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa...

Je! imekwisha kukufikia kwamba usijue la kufanya ili kufariji mtu fulani aliyekuwa amepoteza mpendwa katika kifo?​—Ukurasa 26, mafungu 2-5; Yn. 5:28, 29; km-SW 8/97 ukurasa 8.

Doit-on croire en la Trinité ?

Je! unafikiri kwamba linaweza kuwa jambo lenye mafaa kwa ajili ya wakati wetu ujao kujua utu wa kweli wa Mungu?​—Ukurasa 3, mafungu 3, 7-8; Yn. 17:3.

3 Broshua Zingine: Nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Machi 1998 inatoa orodha ya broshua na vichapo vingine kwa niaba ya Wabudha, Wahindu, Wayahudi na Waislamu. Tunaweza pia kuvitolea, hilo linapoonekana kuwa lenye kufaa. Kwa ajili ya madokezo, turudilie kurasa 4-6 za nyongeza hiyo, vilevile kurasa 21-4 za kitabu Kutoa Sababu, na tutayarishe maonyesho mafupi yanayoamsha kupendezwa kwa watu hao.

4 Broshua nyingine iliandikwa kwa niaba ya wale ambao, ingawa ni wenye elimu, wana ujuzi mdogo juu ya Biblia. Broshua hiyo inalo kusudi la kuwachochea wachunguze Neno la Mungu. Ikiwa nafasi inajitokeza, tunaweza kuitolea:

Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote.

Kulingana na wewe, je! elimu yenye kufaa inapaswa kutia ndani ujuzi fulani juu ya Biblia?​—Ukurasa 3, mafungu 1-3 na ukurasa 30, mafungu 2; Mhu. 12:9, 10.

5 Broshua kwa Ajili ya Funzo: Tungepaswa sikuzote kuwa na mradi wa kuanzisha funzo la Biblia tangu kukutana mara ya kwanza au wakati wa ziara ifuatayo. Kwa hiyo, tunayo broshua inayotuwezesha kuanzisha, kisha kuongoza funzo kwa urahisi:

Mungu Anataka Nini Kwetu.

Je! unajua kwamba kwa kuchukua dakika 30, zikiwa nyingi, kila juma muda wa majuma 16, unaweza kutwaa ujuzi wa msingi wa Biblia?​—Somo 2, fungu 6; 2 Tim. 3:16, 17; km-SW 5/97 ukurasa 8. 

6 Katika kielezi chake cha Msamaria mwema, Yesu alionyesha waziwazi kwamba jirani wa kweli ni yule anayeonyesha upendo na fadhili kuelekea yule anayeteswa. (Lk. 10:27-37) Sasa(yet), wanadamu wenzetu ni wenye kutaabika. Wanahitaji kusikia habari njema. Tutimize wajibu wetu kuelekea jirani yetu kwa kumtangazia habari njema hiyo. Kwa kufanya hivyo, tutakuwa wanafunzi wa kweli wa Yesu Kristo.​—Mt. 24:14; Gal. 5:14.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine