Nataka Funzo la Biblia!
1 Kwa haki, wengi wetu huonyesha tamaa ya kuongoza funzo la Biblia. Ni kwa njia hiyo tunatimiza mradi wetu wa kufanya wanafunzi. (Mt. 28:19, 20) Hata hivyo, wengi wamefanya miezi, hata miaka, bila kupata ile furaha ya kufundisha mtu fulani kweli. Mnamo Novemba, tunaweza kufanya jambo gani ili kutatua tatizo hilo? Kwa kuwa tutatolea kitabu Ujuzi, tutajitahidi kuanzisha mafunzo ya Biblia kupitia kitabu hicho.
2 Weka Kando Mwisho-juma Mmoja au Miwili: Tunatia moyo kila mmoja ajiwekee wakati mnamo mwezi huu ili atafute funzo la Biblia. Viongozi wa Funzo la Kitabu watachagua mwisho-juma au miisho-juma ya kutiwa kando kwa ajili ya utendaji huo, kisha watafanya mipango ili washiriki wa sehemu yao wakaze uangalifu juu ya kufanya ziara za kurudia.
3 Tulete maandishi yetu yanayohusu ziara za kurudia kwenye mikutano yote kwa ajili ya utumishi wa shambani. Kisha, tuende kuona watu wote walioonyesha kupendezwa, waliokubali kichapo au waliohudhuria mikutano. Tufanye kila ziara ya kurudia tukiwa na mradi wa kuanzisha funzo la Biblia.
4 Onyesho la Funzo la Biblia: Wakati wa mikutano kwa ajili ya mahubiri iliyopangwa kuhusiana na utendaji huo, onyesho moja lililotayarishwa vema litafanywa, likionyesha jinsi ya kuanzisha funzo la Biblia wakati wa ziara ya kurudia. Tunaweza kusema: “Watu wengi wanayo Biblia, lakini hawajui kwamba inajibu maulizo ya maana tunayojiuliza maishani. [Tuonyeshe yaliyomo katika kitabu Ujuzi na tusome vichwa vya sura 3, 5, 6, 8 na 9.] Kupitia kitabu hiki kinachosaidia kujifunza, unaweza kupata ujuzi wa msingi wa Biblia kwa muda wa miezi michache tu, ukitumia karibu saa moja kila juma. Ikiwa ungependa kuchagua kimoja cha vichwa hivi, nitakuwa mwenye furaha kukuonyesha jinsi funzo linavyofanywa.” Ikiwa mtu anasita kwa sababu ya programu yake yenye mambo mengi, tumfasirie kwamba tunapendekeza vilevile funzo lenye kufupishwa. Tumtolee broshua Anataka na tupendekeze kuchunguza somo moja fupi la dakika 15 hadi 30 kwa juma.
5 Ikiwa tunajitahidi pamoja ili kuanzisha mafunzo ya Biblia na ikiwa tunamwomba Yehova atubariki, hakika tutapata mafunzo! (1 Yh. 5:14, 15) Ikiwa tunataka kuongoza funzo la Biblia, huu ndiyo wakati wa kulianzisha!