Waangalizi Wanaoongoza—Viongozi wa Mafunzo ya Kitabu
1 Kutumika kama kiongozi wa Funzo la Kitabu ni pendeleo kubwa kwa mzee na mtumishi wa huduma mwenye kustahili. Kushughulikia mahitaji ya kiroho ya wale walio katika kikundi chake ni daraka zito. Wajibu wake ni wa [Meaning: are in]aina tatu.
2 Ufundishaji Wenye Ustadi: Inaomba matayarisho yenye kina kwa kiongozi wa Funzo la Kitabu ili atoe uelewevu kwa kikundi kila juma. Yeye hutafuta kuongeza uthamini wa habari inayochunguzwa. Badala ya kutoa maelezo kupita kiasi yeye mwenyewe wakati wa funzo, atauliza [raise (W 1raise vi 7)]maulizo ya ziada yenye kufaa [pertinent] kwa ajili ya kutokeza mawazo makuu ya somo ikiwa jambo hilo linahitajiwa. Anachopigania ni kufanya funzo liwe lenye kupendeza na lenye kuelimisha na kufanya kila mmoja ashiriki katika mazungumzo. Mradi wake ni kujenga kiroho, kuonyesha manufaa ya funzo, na kufanya habari iguse akili na moyo.—1 Thes. 2:13.
3 Uchungaji Wenye Kusaidia: Kiongozi wa funzo la kitabu ni “kama pahali pa kujificha na upepo, na pahali pa kufunikana na mvua.” (Isa. 32:2) Kwa kweli, yeye hushughulikia wote katika kikundi chake na kuhakikisha kwamba msaada wa kiroho unatolewa wakati mtu fulani kati ya wale walio chini ya uangalizi wake anapovunjika moyo.—Ezek. 34:15, 16; 1 Thes. 2:7, 8.
4 Uenezaji-Evanjeli Wenye Bidii: Kiongozi wa funzo la kitabu ni mwenye bidii katika kufanya mipango yenye manufaa kwa ajili ya wote katika kikundi chake kusudi washiriki kikamili katika huduma ya shambani. Yeye huongoza katika kazi ya kueneza evanjeli, akijua kwamba ukawaida, bidii, na shauku anavyovionyesha katika utumishi vitaonekana kwa wengine katika kikundi. (Kol. 4:17; 2 Thes. 3:9) Kisha, yeye hujitahidi kufanya kazi katika utumishi pamoja na kila mshiriki wa kikundi chake. Ikiwa tunataka kufanya ustadi wetu wa kuhubiri na kufundisha katika huduma uwe bora, kiongozi wa funzo la kitabu anaweza kutusaidia tufikie mradi wetu.—1 Tim. 4:16; 2 Tim. 4:5.
5 Tunabarikiwa kwelikweli kwa kupewa zawadi hizi ambazo ni wanadamu walio tayari kutupa msaada wa kiroho na utegemezo wenye upendo. (1 Thes. 5:14) Kushiriki kwetu kikawaida katika funzo la kitabu na kutegemeza kwetu kwa uaminifu kazi ya kueneza evanjeli na vionyeshe uthamini wetu wa mpango huo wa ajabu kutoka kwa Yehova.—Ebr. 10:25.