Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 2/99 uku. 4
  • Toleeni Watu wa Umri Zote Kitabu Furaha ya Familia

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Toleeni Watu wa Umri Zote Kitabu Furaha ya Familia
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1999
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Tusaidie Familia Kujijengea Wakati Ujao Udumuo
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Tuwajulishe Wengine Siri Ya Kupata Furaha Ya Familia
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Utoaji Uliopendekezwa kwa Ajili ya Utumishi wa Shambani
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Ujuzi Utokao Kwa Mungu Unajibu Kwa Maulizo Mengi
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1999
km 2/99 uku. 4

Toleeni Watu wa Umri Zote Kitabu Furaha ya Familia

1 Kijana mwanamume mwenye umri wa miaka 11 kutoka Kalifornia alionyesha uthamini wake kuhusu kitabu Siri ya Kupata Furaha ya Familia. Aliandika: “Mimi ni mwenye shukrani kuhusu kitabu hicho, nami natia moyo familia zingine zikisome kwa kuwa ni kizuri ajabu. Kinasaidia pia familia yangu ipate amani na furaha katika nyumba yetu.” Jambo lililoonwa la kijana huyo lingepaswa lituchochee tuwatolee watu wa umri zote kitabu Furaha ya Familia. Haya ni madokezo machache unayoweza kujaribu katika huduma yako mnamo Februari:

 2 Unapokutana na kijana, unaweza kusema:

◼ “Vijana wengi wenye umri wako ni wenye kufikiria ndoa. Lakini, ni wapi tunaweza kupata habari yenye kutegemeka kuhusu jambo hilo? [Acha mtu ajibu.] Mara nyingi vijana husema kwamba hawana hakika ikiwa wako tayari kwa ajili ya ndoa. Niruhusu nishiriki nawe yale kitabu hiki kinasema kuhusu habari hiyo.” Fungua kitabu Furaha ya Familia kwenye ukurasa 14, na soma fungu 3. Kisha onyesha kila kichwa kidogo katika sura hiyo. Mtolee mtu kitabu, na fanya mipango kwa ajili ya kurudi.

 3 Unapokutana na mzazi, unaweza kusema:

◼ “Tunashiriki na wazazi mwongozo fulani wenye manufaa unaosaidia kulea watoto. Mwongozo huo umekusanywa katika kitabu hiki Siri ya Kupata Furaha ya Familia.” Fungua kitabu kwenye ukurasa 55. Soma fungu 10 pamoja na andiko la Kumbukumbu la Torati 6:​6, 7, katika fungu 11. Kisha, onyesha sentensi zinazoandikwa katika italiki kwenye mafungu 12 hadi 16. Endelea kwa kusema: “Kitabu hiki kimesaidia wazazi wengi wafanikiwe zaidi. Ikiwa ungetaka kukisoma, nitakuwa mwenye furaha kukuachia nakala hii.”

 4 Unapozungumza na mtu mzee-mzee, unaweza kusema:

◼ “Nitakapomaliza kusoma maelezo haya mafupi, tafadhali nijulishe unawaza nini.” Kwenye fungu 17, soma sentensi mbili za kwanza kwenye ukurasa 169 wa kitabu Furaha ya Familia. Kisha mwombe mtu ajibu. Kulingana na jibu, unaweza kusoma sehemu nyinginezo kutoka kitabu kabla ya kukitoa kwa mtu.

 5 Unaporudi kuwaona wale uliowaachia kitabu Furaha ya Familia, uwe na mradi wa kujaribu kuanzisha funzo la Biblia. Somo 8 katika broshua Anataka au sura 15 katika kitabu Ujuzi vyaweza kuwa nafasi zenye kufaa ili kuanzisha funzo hilo. Wakati uohuo, acheni tujitahidi kusaidia watu wa umri zote wajenge maisha ya Kikristo ya familia yenye furaha.

[DO NOT SET] References

1. g98 2/22 32

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine