Tuwajulishe Wengine Siri Ya Kupata Furaha Ya Familia
1 Familia ndicho kiini cha msingi cha jamii ya kibinadamu, sehemu ya msingi ya miji midogo, miji mikubwa, Shirikisho na mataifa mazima. Leo kuliko wakati mwingine, familia zinashambuliwa. Nguvu zenye uwezo zinashambulia kufikia hata kuwako kwa maisha ya familia. Sisi ni wenye shukrani kama nini kwa Yehova, Mwanzilishi wa familia, kwa kutufundisha ili kwamba tupata furaha ya familia! Wale wanaotumikisha mashauri yake wanaona kwamba matatizo yanapunguka na wanafikia umoja wa familia. Mnamo Oktoba, tunayo shangwe kuangusha kitabu Siri ya Kupata Furaha ya Familia. Tuchukue hatua ya kuwakaribia watu ili kuzungumza nao juu ya maisha ya familia. Tuwe wenye urafiki, wenye kutazamia mema na tuonyeshe utambuzi. Tungeweza kusema nini?
2 Tungeweza kutokeza ulizo kama hili:
◼ “Je! umeona kwamba familia nyingi zinavumilia kwa magumu mikazo ya maisha? [Tuache mtu ajibu.] Inaonekana kwamba watu wengi wana magumu nyumbani. Kulingana nawe, nini kingeweza kusaidia familia kuwa zenye utulivu zaidi na zenye furaha zaidi? [Tuache mtu ajibu.] Kwa kuwa Mungu ndiye Mwanzilishi wa familia, je! lisingekuwa jambo la hekima kuchunguza mashauri anayotutolea kwa upande huo? [Tusome 2 Timotheo 3:16, 17.] Mafundisho hayo ambayo ni kwa faida yetu yanaonyeshwa katika kitabu hiki, Siri ya Kupata Furaha ya Familia.” Baadaye, tumuulize mtu kile ambacho, kulingana naye, kwa kawaida, ni tatizo katika familia, tuonyeshe sura moja inayofasiria ulizo na tumtolee kitabu.
3 Wakati wa ziara ya kurudia, kwa kuwa kusudi letu ni kuanzisha funzo la Biblia, tungeweza kusema:
◼ “Nilifikiri kwa yale uliyoniambia kuhusu maisha ya familia, na nilikuletea kitu fulani ambacho ungeweza kuthamini. [Tuonyeshe broshua Anataka, tufungue ukurasa 16 na tusome maulizo sita yanayoulizwa juu ya ukurasa.] Kwa haki, kila mshiriki wa familia anapaswa kutimiza sehemu yake ili kuchangia furaha ya familia. Ikiwa una dakika chache tu, ningekuonyesha jinsi ya kufaidika na yale yanayosemwa hapa.” Tuanze sasa kujifunza somo la 8.
4 Njia nyingine ya kuanzisha mazungumzo ni kutaja tatizo fulani, kwa kusema jambo fulani kama hili:
◼ “Ingawa kila mmoja anataka kuridhika na kutosheka, yaelekea kwamba familia nyingi hakika hazifikii hilo. Kulingana nawe, nini ingeweza kuzisaidia kupata furaha ya kweli? [Tuache mtu ajibu.] Tangu zamani, Biblia ilifunua ni aina gani ya matatizo ambayo familia zingepambana nayo leo. [Tusome 2 Timotheo 3:1-3.] Hata hivyo, Biblia inafasiria pia familia jinsi ya kufanya ili kutatua matatizo yao na kupata furaha yenye kudumu. Hilo linaonyeshwa katika kitabu hiki, Siri ya Kupata Furaha ya Kweli.” Baadaye, tuvute uangalifu wa mtu juu ya maulizo ya kujikumbusha mwishoni mwa sura inayopatana, tuyasome, na tutolee kitabu.
5 Wakati wa ziara ya kurudia, tutumie broshua “Anataka” ili kuanzisha funzo. Tungeweza kusema:
◼ “Nilithamini sana tamaa yako ya kuchunguza kanuni za Biblia zinazogusa maisha ya familia. Ujuzi wa mambo unaonyesha kwamba tunapata matokeo bora kwa kufuata mashauri yenye kutenda kazi yaliyomo katika Biblia. Tazama kwa urahisi sababu.” Tusome fungu la kwanza la somo la 1 katika broshua Anataka, kutia ndani Zaburi 1:1-3 au Isaya 48:17, 18. Ikiwa hali zinaruhusu, tuchunguze somo lote. Tupendekeze kurudi kuzungumza juu ya somo lifuatalo.
6 Kuhusu Vichapo Vyetu: adaptation RDC ? ? Tujuapo kwamba vichapo vyetu ni vyenye thamani na kwamba kutolewa kwavyo ni kwa bei ghali, je! inatufikia kusita kutolea magazeti, broshua au vitabu kwa watu ambao tunakutana nao? Jinsi gani tunaweza kuwa hakika kwamba hatuachi vichapo vyetu kwa watu ambao hawavithamini? Njia moja ni kumuuliza mtu ikiwa anatuhakikishia kwamba atasoma kichapo ambacho tunamtolea.
7 Tunapotolea kitabu “Furaha ya Familia,” kwa mfano, tungeweza kusema hivi:
◼ “Ikiwa unaniambia kwamba utasoma kitabu hiki, ninakuachia chenyewe kwa mchango mdogo. Labda unapendezwa kujua kwa nini tunaomba mchango mdogo. Sababu ni kwamba kazi yetu inategemezwa na michango ya kujipendea. Michango yenu inatuwezesha tu kulipia gharama za usafirishaji. Kwa hiyo nitafurahi kukuachia kitabu hiki ambacho kitakusaidia kuvumbua siri ya kweli ya kupata furaha ya familia na nitakuachia chenyewe kwa mchango mdogo wa . . . [Tuonyeshe bei ya sasa.]”
8 Tufanye yote tuwezayo ili kuwajulisha wengine siri inayoongoza kwenye furaha ya familia: utii kwa maagizo yanayoonyeshwa katika Neno la Mungu.—Zab. 19:7-10.