Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 4/97 uku. 8
  • Tusaidie Familia Kujijengea Wakati Ujao Udumuo

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Tusaidie Familia Kujijengea Wakati Ujao Udumuo
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Toleeni Watu wa Umri Zote Kitabu Furaha ya Familia
    Huduma Yetu ya Ufalme—1999
  • Tuwajulishe Wengine Siri Ya Kupata Furaha Ya Familia
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Utoaji Uliopendekezwa kwa Ajili ya Utumishi wa Shambani
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Ujuzi Utokao Kwa Mungu Unajibu Kwa Maulizo Mengi
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1997
km 4/97 uku. 8

Tusaidie Familia Kujijengea Wakati Ujao Udumuo

1 “Pupa ni yenye manufaa, alisema mwanauchumi mmoja kwa wahitimu wa chuo kikuu cha Amerika. Mtu anaweza kuwa mwenye pupa na kujisikia vizuri mwilini mwake.” Hayo ndiyo maoni hasa ya ulimwengu, ambapo uchoyo unaonyeshwa kama njia ya mtu kujijengea wakati wake ujao. Kinyume na hilo, Yesu alifundisha kwamba Mkristo anapaswa ‘kujikana mwenyewe, kwa maana itakuwa manufaa gani kwa mtu ikiwa atapata faida ya kuwa na ulimwengu wote lakini aipoteze nafsi yake?’ (Mt. 16:​24-26, TUM) Ili kujijengea wakati ujao wenye kudumu, inaomba mtu kutegemeza maisha yake yote katika utimizo wa mapenzi ya Mungu, jambo ambalo linapaswa kuwa ndio mradi wa lazima wa familia leo. (Zab. 143:10; 1 Tim. 4:8) Ndilo wazo linalotolewa na sura ya mwisho ya kitabu Furaha ya Familia. Kitabu hicho kipya kinawezesha watu kuona jambo ambalo ni la muhimu hakika katika maisha na jinsi ya kutenda kwa namna yenye kujenga kuelekea familia zao. Tunapoendelea kuhubiri habari njema popote, tunaweza kusema nini ili kuwatia moyo wale ambao tunakutana nao kusoma kitabu Furaha ya Familia? Angalia madokezo fulani:

2 Milangoni au barabarani, tunaweza kujaribu kuanzisha mazungumzo kwa msaada wa trakti “Maisha ya Familia Yenye Furaha.” Tunaweza kuuliza hivi:

◼ “Maisha ya sasa ni chanzo cha mahangaiko mengi, lakini unafikiri kwamba inawezekana hata hivyo kuwa hakika na maisha ya familia yenye furaha? [Tuache mtu aseme.] Trakti hii inatuhakikishia kwamba ndiyo. Je! ungependa kuisoma?” Ikiwa mtu anakubali, tungeweza kuendelea hivi: “Kwa kuwa habari hii inakupendeza, labda ungethamini pia kitabu hiki kinachotoa mashauri kamili juu ya njia ya kupata furaha katika mazingira ya kifamilia.” Tuonyeshe mambo yaliyomo ya kitabu Furaha ya Familia. Tuonyeshe sura fulani fulani zenye kichwa cha habari chenye kuvutia. Tufungue kitabu kwenye ukurasa wa 10 na tusome sentensi ya mwisho ya fungu la 17 na pia fungu la 18 lote. Tutolee kitabu kwa kuonyesha bei ya sasa. Tumfasirie mtu kwamba tutaweza kuzungumzia ulizo hilo kirefu zaidi na tumuulize wakati gani ingewezekana kumuona tena.

 3 Tungeweza kuendeleza mazungumzo kuhusu maisha ya familia yenye furaha kwa kusema haya yafuatayo:

◼ “Ningependa kuvutia uangalifu wako juu ya wazo linalopatikana katika kitabu ambacho nilikuachia; ninafikiri kwamba hilo litakufurahisha. Sura ya mwisho inazungumzia siri ya furaha ya familia. [Tusome fungu la 2 la ukurasa 183.] Angalia kwamba ufunguo wa furaha ni kutumika pamoja kwa utimizo wa mapenzi ya Mungu. Tunapendekeza kwa watu kujifunza Biblia katika familia ili kuendelea kutwaa ujuzi wa mapenzi ya Mungu na kuyatumikisha nyumbani. Tunatolea funzo la Biblia la bure linalodumu tu miezi fulani. Ikiwa unaniruhusu hivyo, nitakuonyesha jinsi linavyofanyika.” Turudi tena pamoja na broshua Mungu Anataka Nini Kwetu? au kitabu Ujuzi, kwa kuchagua kile kifaacho.

 4 Ikiwa tunazungumza na marafiki wa darasa letu shuleni au pamoja na vijana katika eneo, tungeweza kutokeza ulizo lifuatalo:

◼ “Ni nini ulazima kwa wazazi na watoto wao kudumisha mawasiliano kati yao? [Acha mtu ajibu.] Tuangalie yale kitabu hiki kinasema kuhusu ‘mawasiliano ya haki na yaliyo wazi.’ [Tusome fungu la 4 lote na sentensi ya kwanza ya fungu la 5 la ukurasa 65 wa kitabu Furaha ya Familia.] Mafungu yafuatayo yanatoa madokezo yenye kutenda kazi juu ya namna ya kurekebisha mawasiliano katika familia. Kitabu hiki ni chenye kichwa Siri ya Kupata Furaha ya Familia. Ikiwa unataka kupata kitabu na unatamani kweli kukisoma, ninaweza kukuachia chenyewe, kwa msaada wa mchango mdogo wa. . . .” Tufasirie kwa msikilizaji wetu kwamba tungependa kumuona tena ili kujua maoni yake juu ya yale atakayosoma.

 5 Tungeweza kujenga juu ya msingi wa mazungumzo yetu ya kwanza pamoja na kijana kuhusu mawasiliano kati ya wazazi na watoto kwa kusema hivi:

◼ “Nilithamini kwamba unashikilia sana ulazima wa mawasiliano mazuri katika mazingira ya kifamilia. Kulingana nawe, ni nini kichwa cha habari kilicho cha lazima zaidi ambacho wazazi na watoto wangepaswa kuzungumzia?” Tuache mtu ajibu. Tufungue baadaye kitabu Furaha ya Familia kwenye ukurasa 68 na tusome jibu ambalo hutolewa na sehemu ya kwanza ya fungu la 11. “Njia yenye matokeo zaidi ya kutwaa ujuzi wa Mungu ni kujifunza Biblia kila juma.” Tutolee broshua Mungu Anataka Nini Kwetu? Tufasirie kwamba masomo 16 yaliyomo yanaonyesha mistari muhimu ya yaliyomo katika Biblia. Tusome utangulizi unaopatikana kwenye ukurasa wa 2 na tuchunguze pamoja na mtu somo la kwanza.

 6 Ikiwa, katika mlango kwa mlango, au labda katika shule au sokoni, tunakutana na baba au mama wa familia, tungeweza kuamsha kupendezwa kwake kwa kusema:

◼ “Nipo hakika kwamba unakubaliana nami ili kusema kwamba ni vigumu sana kulea watoto leo. Kulingana nawe, nini kinachoweza kulinda familia yako na mavutano mabaya? [Tuache mtu ajibu.] Angalia mashauri yenye hekima ambayo mimi mwenyewe niliweza kuyathamini.” Tuvutie uangalifu juu ya kielelezo kinachotolewa kwenye ukurasa wa 90 wa kitabu Furaha ya Familia, katika fungu la 1, na tusome fungu la 2. Tuonyeshe katika nini madokezo yenye usawaziko yanayotolewa na kitabu hicho ni yenye kutenda kazi ili kulinda familia dhidi ya mavutano mabaya. Tupendekeze kwa mtu kumwachia nakala moja na kumuona tena ili kujibu kwa maulizo ambayo angeweza kutokeza.

 7  Tunaporudi kumuona tena baba au mama wa familia aliyekubali kitabu “Furaha ya Familia,” tunaweza kuendeleza mazungumzo kwa namna ifuatayo:

◼ “Mara ya mwisho tulipoonana, niliweza kutambua kwamba unahangaikia kweli kweli watoto wako na kwamba unataka kufanya yote uwezayo ili kuwalinda dhidi ya uvutano mbalimbali mbaya. Labda haujasoma bado kitabu ambacho nilikuachia, lakini kina wazo moja lenye kupendeza ambalo ningependa kukuonyesha. [Tusome fungu la 19 la ukurasa wa 59.] Ili kuanzisha uhusiano pamoja na Mungu, tunapaswa kujifunza kumjua kwa njia ya Neno lake lililoandikwa, Biblia. Je! ungependa kwamba nikuonyeshe jinsi tunavyojifunza Biblia katika familia?”

 8 Katika ulimwengu, washauri hawawezi kuonyesha familia njia ya furaha; kuna hatari waweze kuzikatisha tamaa. Tutolee kwa uwingi kitabu Furaha ya Familia, ili kwamba Neno la Mungu liweze kuwasaidia watu wa aina zote kujijengea wakati ujao wenye kudumu.—1 Tim. 6:19.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine