Pangeni Kimbele!
1 Tengenezo la Yehova hutuandalia programu ya kawaida ya utendaji mbalimbali wa kitheokrasi ambao hutimiza mahitaji yetu ya kiroho. Kuwa wenye shukrani hutusukuma tufaidike kikamili na mambo yote yaliyopangwa, kama vile ziara za waangalizi wasafiri, mikusanyiko na makusanyiko, na utendaji mwingine mbalimbali wa pekee unaopangwa mahali petu. (Mt. 5:3) Hata hivyo, wengine hukosa kufaidika na mengi ya maandalizi hayo kwa sababu ya mipango mingineyo waliyoifanya. Ni nini linaloweza kufanywa ili kuzuia jambo hilo? Tunawezaje kuhakikisha kwamba utendaji usio wa kitheokrasi hausongi “mambo yaliyo ya maana zaidi,” ambayo yangepaswa kuorodheshwa kwanza kwenye programu ya kila Mkristo?—Flp. 1:10.
2 Kupanga Kihekima Ni kwa Lazima: Mezali 21:5 laonya: “Mafikili ya wenye bidii yanaelekea utajiri tu, lakini kila mutu anayetenda kwa haraka anaelekea uhitaji.” Ili kupata “utajiri” wa kiroho, tunahitaji kupanga kimbele kwa uangalifu, tukikumbuka utendaji mbalimbali wa kitheokrasi uliopangwa. Tungepaswa kupanga utendaji wetu wa binafsi wakati ambapo hautazuia kuhudhuria kwetu ili kuvuna baraka za kiroho. Ikiwa tunafanya mipango kwa haraka ili kufanya mambo ambayo sisi binafsi twataka kufanya, bila kufikiria matukio ya kitheokrasi yanayokaribia, yaelekea tutapata “uhitaji” wa kiroho.
3 Usikose! Sisi sote hufanya mipango kwa ajili ya wakati ujao, kutia ndani likizo, safari za biashara, matembezi pamoja na washiriki wa familia, na kadhalika. Kabla ya kujifunga wajibu au kukamilisha mipango yako, ona programu ya utendaji mbalimbali wa kiroho unaokaribia. Ukiona kwamba mwangalizi wa mzunguko atakuja au kwamba mkusanyiko unapangwa wakati uleule utakapokuwa katika safari, jitahidi sana kupanga upya mambo yako ili ushiriki. Twajulishwa kimbele sana kuhusu matukio makubwa yanayopangwa kwa ajili ya wakati ujao. Wazee wa kutaniko lenu waweza kuwajulisha mambo yaliyopangwa mahali penu.
4 Kwa kudhihirisha busara na kupanga kimbele kwa ajili ya mambo yaliyo ya maana zaidi, tutakuwa wenye “kujazwa matunda ya uadilifu, . . . kwa utukufu na sifa ya Mungu.”—Flp. 1:11.