Majibu ya maulizo yenu
◼ Ni vichapo gani ambavyo tungepaswa kujifunza na wapya kabla ya ubatizo wao?
Kabla ya mtu kuweka maisha yake wakfu kwa Yehova na kubatizwa, yeye anapaswa kutwaa ujuzi sahihi. (Yn. 17:3) Atapata habari anayoihitaji kwa kujifunza broshua Mungu Anataka Nini Kwetu? na kitabu Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele. Katika visa vilivyo vingi zaidi, mwanafunzi atajifunza kwanza broshua Anataka. Hata hivyo, ikiwa funzo lilianzishwa katika kitabu Ujuzi, ingefaa kujifunza broshua Anataka baada ya kumaliza kitabu. Kwa nini jambo hilo lahitajiwa?
Broshua Anataka inaandaa mwono wa jumla wa mafundisho ya msingi ya Biblia. Ikiwa mwanafunzi anajifunza broshua hiyo kwanza, hiyo itamtolea uelewevu wa msingi wa mambo yanayotakwa ili kumpendeza Yehova. Ikiwa anajifunza hiyo baadaye, hiyo itatumika kuwa kujikumbusha kuzuri mambo yaliyozungumziwa katika kitabu Ujuzi. Katika hali zote mbili, mtie moyo mwanafunzi achunguze maandiko yanayotegemeza mawazo, na atafakari juu ya hayo. Hakikisha kwamba unatia mkazo juu ya picha, kwa kuwa hizo ni misaada yenye matokeo sana katika kufundisha.—Ona Mnara wa Mlinzi wa Januari 15, 1997, kurasa 16-17.
Mwanafunzi anapokamilisha funzo la vichapo hivyo viwili, labda anaweza kujibu maulizo yote ambayo wazee watarudilia pamoja naye ili kumtayarisha kwa ajili ya ubatizo. Ikiwa ni hivyo, huenda lisiwe jambo la lazima kuongoza funzo la kawaida pamoja naye katika kichapo kingine, ingawa kiongozi angepaswa aendelee kupendezwa sana na maendeleo yake.—Ona Mnara wa Mlinzi wa Januari 15, 1996, kurasa 14, 17.