Tusaidie Watu Wasio Na Ujuzi Kuelewa
1 Kwa msaada wa kazi ya kufanya wanafunzi, tunafundisha watu wengine yale Mungu anataka kwao. (Mt. 28:19, 20) Kwa upande huo, juhudi kubwa inafanywa ulimwenguni pote na zaidi ya milioni tano ya Mashahidi. Mafanikio hayatokani na hesabu ya saa, vitabu vilivyoangushwa au mafunzo ya Biblia yaliyoanzishwa. Tunafikia mradi wetu wakati watu wanapoelewa na kutenda kupatana na yale waliyojifunza.
2 Ili kuwasaidia kwa upande wa kiroho, inafaa ‘kuwaelewesha watu wasio na ujuzi.’ (Zab. 119:130) Moyo wao unaguswa na wanasukumwa kutenda ikiwa tu ‘wanaelewa maana.’ (Mt. 15:10) Kwa kadiri kazi yetu inakuwa kubwa na kupanuka, tunatambua vizuri zaidi ulazima wa kusema na kufundisha kwa urahisi. Ni kwa sababu hiyo Sosaiti ilitoa broshua Mungu Anataka Nini Kwetu? Inatoa masomo kamili kuhusu mafundisho ya msingi ya Biblia. Sura ni fupi, usemi ni mwepesi, na mafundisho mepesi kueleweka, jambo ambalo linafanya broshua hiyo iwafikie watu wengi.
3 Mnamo Mei na Juni, zaidi ya magazeti tutaitolea pia broshua hiyo. Tutakapojitayarisha kwa ajili ya juma letu la mahubiri, tunashauriwa kujitayarisha kutolea magazeti Siku ya Posho na kutumia broshua siku zinazobaki za juma. Tuitolee kwa wale ambao tayari wamekwisha kukubali vitabu wakati wa nyuma. Tukumbuke kwamba inaweza kuwa yenye manufaa ili kuwafundisha watoto, watu wa lugha ya kigeni na wale walio na matatizo ya kusoma.
4 Tuwafikie Watu kwa Urahisi: Tunapotolea broshua Anataka, tujielekeze kwenye ukurasa wa 2 ambako inafasiriwa kwamba broshua hii “imetayarishwa kwa kusudi la kutoa funzo la Biblia.” Tuvutie uangalifu kwenye fungu la 3, ukurasa 3, ili kumuonyesha mtu kwa nini anahitaji kujifunza Biblia. Tuamshe kupendezwa kwake kwa msaada wa kichwa cha sura fulani zinazoonyesha kweli nyepesi za Biblia. Tumuonyeshe kwamba broshua hii inafanyiza funzo kuwa lenye kupendeza na tumtolee msaada wetu.
5 Tuongoze Funzo Hatua kwa Hatua: Mradi wetu si tu kuongoza mafunzo, tunataka pia kufanya wanafunzi ambao watakuwa wateteaji mashuhuri wa ibada ya kweli. Broshua inaweza kumalizwa katika majuma fulani, na uchunguzi huo ungepaswa kufikia moja kwa moja kwenye funzo la kitabu Ujuzi (ona taarifa chini ya ukurasa 31). Tangu mwanzoni, tumsaidie mwanafunzi kutambua tengenezo la Yehova. (ona Kutoa Sababu kurasa 314-5.) Tusisitize juu ya thamani ya mikutano ya kutaniko na tufasirie kwamba kuhudhuria kwenye mikutano hiyo huwezesha kuelewa hatua kwa hatua jinsi ya kufuata ibada safi.—Ebr. 10:24, 25.
6 Ni hakika kwamba ikiwa tunashiriki kikamilifu katika utendaji huo wa pekee mnamo Mei na Juni, tutapata shangwe ya kusaidia watu wanyofu ‘kujipatia akili’ iongozayo kwenye uhai.—Mez. 4:5.