Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 9/00 uku. 1
  • Uhai wa ni katika hatari!

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Uhai wa ni katika hatari!
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Tuendelee kuhubiri!
    Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • Unatimiza kwa Ukamili Utumishi Wako?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2019
  • Kufanya Kazi Pamoja na Mungu—Kunaleta Furaha
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2016
  • Tolea Watu Magazeti Yanayotoa Ushahidi Juu ya Ile Kweli
    Huduma Yetu ya Ufalme—2007
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2000
km 9/00 uku. 1

Uhai wa ni katika hatari!

1 Biblia inaonyesha wazi mapenzi ya Mungu “kwamba watu wa namna zote waokolewe.” Hata hivyo, ni kweli pia kwamba matazamio ya uhai ya mamilioni ya watu duniani yanategemea mtazamo wao kuelekea Yehova Mungu na Ufalme wake kupitia Yesu Kristo. Mtazamo wenye kufaa unaweza kuwa na msingi tu juu ya “ujuzi sahihi wa kweli.” (1 Tim. 2:3, 4) Huku tukijulisha watu kwamba karibuni dunia itasafishwa kwa kuondolewa ubaya wote ili kuacha nafasi kwa ulimwengu mpya wa uadilifu wa Mungu, tumeamuriwa pia kufanya kazi ya maana sana ya kuokoa uhai.—Mt. 24:14; 28:19, 20; Rom. 10:13-15.

2 Kwa nini ni ya haraka sana? Yesu alitoa onyo kuhusu “dhiki kubwa ya namna ambayo haijapata kutukia tangu mwanzo wa ulimwengu.” (Mt. 24:21) Dhiki hiyo itafikia mwisho wake kwenye Har–Magedoni. (Ufu. 16:16) Makundi ya watu watakaopatwa na uharibifu ikiwa wanashindwa kuitikia habari njema yanatia ndani watu wa jamaa yetu wasioamini, majirani zetu, wafanyakazi wenzetu, wanashule wenzetu, na watu tunaojuana nao. Lakini hangaiko letu ni kufikia “watu wa namna zote” tukiiga Mungu, ambaye alionyesha upendo wake kwa ulimwengu wote wa wanadamu kwa kutoa Mwana wake, Yesu Kristo, kuwa dhabihu ya ukombozi kwa ajili ya wote. (Yn. 3:16) Tunapaswa kujitahidi kwa bidii kualika wote wakimbilie mahali pa Mungu pa usalama. Kwa kutimiza kikamili kazi ya kuhubiri, tunaweza kuepuka hatia ya damu.—Ezek. 33:1-7; 1 Kor. 9:16.

3 Mradi wetu ni gani? Umaana wa kazi ya kuhubiri unakaziwa tangu mwanzo mpaka mwisho wa Neno la Mungu. Kama ilivyoonyeshwa na mtume Paulo, “upendo alio nao Kristo hutushurutisha” kuishi kulingana na njia za Mungu. (2 Kor. 5:14) Kwa kuongezea, Mnara wa Mlinzi unakazia mara nyingi wajibu wetu wa kuhubiri. Huduma Yetu ya Ufalme inaendelea kutoa mwongozo juu ya jinsi ya kutimiza kazi ya kuhubiri. Wazee wanapanga kazi hiyo na wanatutia moyo kuishiriki. Wahubiri wenzetu wanatualika kushiriki pamoja nao katika huduma. Tunasikia mengi kuhusu kutayarisha utoaji wetu mbalimbali, kutolea watu magazeti na vichapo vingine, kufanya ziara za kurudia, kuongoza mafunzo ya Biblia, na kutumia kila nafasi ili kutoa ushahidi. Hayo yote yanatusaidia kutimiza mradi wa kuokoa uhai.—1 Kor. 9:22, 23; Efe. 1:13.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine