Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 11/00 uku. 1
  • ‘Neno linalosemwa kwa wakati wenye kufaa’

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • ‘Neno linalosemwa kwa wakati wenye kufaa’
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Kuzungumuza kwa Njia ya Kawaida
    Penda Watu—Juu Ufanye Wanafunzi
  • Utoaji mwepesi ni bora zaidi
    Huduma Yetu ya Ufalme—2001
  • Kutangaza “Habari Njema juu ya Yesu”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” juu ya Ufalme wa Mungu
  • Uishi Kulingana na Sala ya Mufano—Sehemu ya 1
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2000
km 11/00 uku. 1

‘Neno linalosemwa kwa wakati wenye kufaa’

1 Je, kushiriki ujumbe wa uhai pamoja na wengine ni tatizo kwako? Je, unafikiri kwamba unapaswa kusema jambo fulani la akili ili kugusa moyo wa wasikilizaji wako? Wakati Yesu alipotuma wanafunzi wake, aliwaambia: “Mukikwenda, hubirini mukisema: Ufalme wa mbinguni ni karibu.” (Mt. 10:7, ZSB) Ujumbe huo ulikuwa mwepesi kueleweka na rahisi kushiriki. Mambo ni hivyohivyo leo.

2 Mara nyingi, ni maneno machache tu ndiyo yanahitajiwa ili kuanzisha mazungumzo. Wakati Filipo alipokutana na towashi Mwethiopia, yeye alimwuliza: “Je, wewe kwa hakika wajua unayoyasoma?” (Mdo. 8:30) Ni mazungumzo yenye kuthawabisha kama nini ambayo yalitokana na ‘neno lililosemwa kwa wakati wenye kufaa’!—Mez. 25:11.

3 Unaweza kutumia njia yenye kufanana na hiyo katika huduma yako. Namna gani? Kwa kuwa mtazamaji mwangalifu na kuchagua maneno yenye kupatana na hali. Uliza ulizo, na usikilize jibu.

4 Maulizo fulani ya msingi: Ili kuanzisha mazungumzo, unaweza kujaribu lolote la maulizo haya:

◼ “Je, unatumia Sala ya Bwana (au, Baba Yetu) katika ibada yako?” (Mt. 6:9, 10) Sema kutoka moyoni sehemu ya sala hiyo, na kisha uongeze: “Watu fulani huuliza, ‘Jina la Mungu ambalo Yesu alisema linapaswa kutakaswa (au kutukuzwa) ni gani?’ Wengine huuliza, ‘Ni nini ule Ufalme ambao Yesu alisema tunapaswa kusali kwa ajili ya huo?’ Je, umepata majibu yenye kutosheleza kwa maulizo hayo?”

◼ “Je, umepata kujiuliza: ‘Ni nini maana ya uhai?’ ” Onyesha kwamba maana hiyo inahusiana na ujuzi fulani juu ya Mungu.—Mhu. 12:13; Yn. 17:3.

◼ “Je, unafikiri kwamba kifo kitaondolewa wakati wowote?” Tumia Isaya 25:8 na Ufunuo 21:4 ili kutoa jibu lenye kutumainika.

◼ “Je, kuna suluhisho jepesi kwa msukosuko katika ulimwengu?” Onyesha kwamba Mungu anafundisha “umpende jirani yako.”—Mt. 22:39.

◼ “Je, msiba wa kutoka nje ya dunia utaharibu dunia yetu siku fulani?” Shiriki ahadi ya Biblia ya kwamba dunia itadumu milele.—Zab. 104:5.

5 Toeni habari njema kwa namna nyepesi na ya moja kwa moja. Yehova atabariki jitihada zenu za kushiriki hata ‘neno moja’ la kweli pamoja na wengine.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine