Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
MNARA WA MLINZI Nov. 15
“Tumesikia maneno ‘Yesu alikufa kwa ajili yetu.’ [Taja moja kwa moja maneno ya Yohana 3:16.] Je, umepata kujiuliza jinsi kifo cha mtu mmoja kinavyoweza kutuokoa sote? [Acha mtu ajibu.] Biblia inatoa jibu jepesi. Makala hii, ‘Yesu Huokoa—Jinsi Gani?’ inalifafanua waziwazi.”
Amkeni! Nov. 22
“Je, wanadamu wanafanya yote wawezayo ili kulinda mazingira? [Acha mtu ajibu.] Wengi hujiuliza ikiwa ule usawaziko unaoweza kuvurugika kwa vyepesi wa maisha duniani utadumu milele. Jambo lenye kufurahisha ni kwamba Mungu anapendezwa sana na usawaziko huo. [Soma Nehemia 9:6.] Gazeti Amkeni! linazungumzia kile ambacho wakati ujao unawekea maisha duniani.”
MNARA WA MLINZI Des. 1
“Wakati huu wa mwaka, watu wengi wanajishughulisha na kutoa zawadi na matendo mengine mema. Hilo linakumbusha ile Kanuni Iliyo Bora. [Soma Mathayo 7:12.] Je, unafikiri inawezekana kuishi kulingana na kanuni hiyo mwaka wote mzima? [Acha mtu ajibu.] Gazeti hili linatoa mambo mengi ya kufikiria kuhusu ‘Ile Kanuni Bora—Je, Bado Inafaa?’ ”
Amkeni! Des. 8
“Biblia inaahidi kwamba kutakuwa siku ambapo hakuna mtu atakayeweza kusema, ‘Mimi ni mgonjwa.’ [Soma Isaya 33:24.] Kwa kupatana na ahadi hiyo, toleo hili la Amkeni! linakaza uangalifu juu ya ugonjwa unaotesa mamilioni ya watu, vijana na wazee. Ni lenye kichwa ‘Tumaini kwa Wale Wanaougua Yabisi-Kavu.’ Nina hakika kwamba utaona makala hizi kuwa zenye kuelimisha.”