Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
MNARA WA MLINZI Juni 15
“Je, unafikiri kwamba matatizo kama haya yatakwisha wakati wowote? [Soma mtajo wa kwanza wa makala ya kwanza, na uache mtu ajibu.] Neno la Mungu lililoandikwa kwa uongozi wa roho yake linatuhakikishia kwamba matatizo kama hayo yatakwisha karibuni. [Soma Zaburi 72:12-14.] Toleo hili la Mnara wa Mlinzi linaeleza jinsi jambo hilo litakavyotimizwa.”
Amkeni! Juni 22
“Je, unafikiri kwamba uhuru wa kweli utawezekana wakati wowote kwa kila mtu duniani? [Acha mtu ajibu.] Ona ahadi hii nzuri ya Mungu. [Soma Waroma 8:21.] Ili ahadi hiyo itimizwe, lazima utumwa wote uishe, sivyo? Toleo hili la Amkeni! linaonyesha jinsi jambo hilo litakavyotukia.”
MNARA WA MLINZI Julai 1
“Mamilioni ya watu wanatumia mifano au sanamu katika ibada yao, huku mamilioni ya wengine wakifikiri kwamba kufanya hivyo ni kosa. Je, umekwisha kujiuliza Mungu anafikiri nini? [Acha mtu ajibu. Kisha, soma Yohana 4:24.] Makala hizi zinaonyesha jinsi matumizi ya sanamu yalivyoanza, na yale ambayo Biblia inasema kuhusu ibada ya sanamu.”
Amkeni! Julai 8
“Biblia ilitabiri kwamba kungekuwa nyakati ngumu katika siku za mwisho. [Soma 2 Timotheo 3:1, 3.] Ulimwenguni pote, viwango vya uhalifu vinatoa uhakikisho wa jambo hilo. Hali zingalikuwa mbaya zaidi kama nini ikiwa kusingalikuwa polisi! Toleo hili la Amkeni! linazungumzia matatizo ambayo polisi wanapambana nayo ulimwenguni pote.”