Onyesha Uthamini Kuelekea Mali ya Kitheokrasi
1 Alipokuwa akichukua mipango ili kutengeneza hekalu, Mfalme Yosia alisifu wale waliopewa mgawo wa kufanya kazi, akisema: “Hawakuulizwa habari za ile feza waliyoipokea; maana walitenda kazi kwa uaminifu.” (2 Fal. 22:3-7) Uthamini ambao wanaume hao walikuwa nao kuelekea vitu vitakatifu ulionekana wazi kupitia jinsi walivyoshughulika na mali waliyopewa. Leo, tunaposhiriki kazi takatifu ya habari njema ya Mungu, sisi pia tunahitaji kuonyesha uaminifu katika kushughulika na mali tuliyopewa.
2 Katika Huduma ya Shambani: Kuelewa umaana wa ujumbe unaopatikana katika vichapo vyetu na gharama zinazohusika katika utoaji wa vichapo hivyo kunatufanya tuvithamini sana. Hatupaswi kutoa vichapo vyetu ovyoovyo kwa wale ambao hawaonyeshi uthamini wa kweli kuelekea ujumbe wa Biblia. Ikiwa mtu hapendezwi kabisa na habari njema, labda tutamtolea trakti badala ya kichapo kingine.
3 Gawa vichapo katika njia itakayoonyesha kwamba unaheshimu thamani yavyo. Epuka kuviacha katika maeneo ya watu wote ambapo vitasambazwa ovyoovyo. Ili uepuke kupoteza vichapo, fanya hesabu ya vile ulivyo navyo nyumbani kabla ya kupata vingine. Ikiwa kwa kawaida una hesabu ya ziada ya kila toleo la magazeti, fikiria kupunguza ombi lako.
4 Vichapo kwa Ajili ya Matumizi ya Kibinafsi: Tunapaswa kufanya tu ombi la vichapo tunavyohitaji kwelikweli. Tunapaswa kuwa na kiasi hasa tunapoomba Bibles de luxe, Bibles avec références, na vichapo vingine vikubwa-vikubwa, kama vile Concordance, Index, mabuku ya Étude perspicace, na kitabu Wapiga-Mbiu; uchapishaji wa vichapo hivyo vyote unaomba gharama kubwa.
5 Je, unakumbuka kuandika jina lako na anwani yako katika nakala zako binafsi za vichapo? Jambo hilo linasaidia kupunguza uhitaji wa kupata vichapo vitakavyochukua nafasi ya vile vilivyowekwa mahali pasipofaa. Ikiwa unapoteza kitabu cha nyimbo, Biblia, au kitabu cha funzo, labda utakipata kati ya vitu vilivyopotea na kukusanywa kwenye Jumba la Ufalme au mahali pa kusanyiko.—Luka 15:8, 9.
6 Na tujitahidi kutumia vichapo vyetu kwa hekima. Hiyo ni njia ya kuonyesha uaminifu wetu katika kushughulika na mali ya Ufalme ambayo Yehova ametutolea.—Luka 16:10.