Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 12/11 uku. 2
  • Kisanduku Cha Maulizo

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Kisanduku Cha Maulizo
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2011
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Tutumie Vichapo Vyetu kwa Hekima
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2017
  • Fanya Matumizi Yenye Hekima ya Vichapo Vyetu Vyenye Kutegemea Biblia
    Huduma Yetu ya Ufalme—2005
  • Kutolea Watu Vichapo Katika Eneo Ambamo Lugha Nyingi Zinasemwa
    Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • Je, Kichapo Hiki Kinafaa?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2011
Huduma Yetu ya Ufalme—2011
km 12/11 uku. 2

Kisanduku Cha Maulizo

◼ Ni jambo gani litatusaidia kujua ikiwa tutamuachia mutu fulani vichapo vyetu?

Jambo la maana zaidi ni kuona ikiwa mutu anapendezwa. Ikiwa anapendezwa kwelikweli, tunaweza kumuachia magazeti mawili, ao broshua, ao kitabu, ao kichapo kingine chochote tunachotolea watu mwezi huo. Tutamwachia kichapo hata ikiwa tunatambua kwamba hana feza za kutoa kwa ajili ya kazi ya ulimwenguni pote ao hata ikiwa feza zake ni chache. (Ayu. 34:19; Ufu. 22:17) Lakini, vichapo vyetu ni vya maana sana, hatupaswi kuviachia watu ambao hawavioni kuwa vya maana.—Mt. 7:6.

Ni nini kitatusaidia kuona ikiwa mutu anapendezwa? Ikiwa mutu anafurahia kuzungumuza nasi ni alama nzuri. Ikiwa mutu anatusikiliza tunaposema, anajibu tunapomuuliza maulizo, na anatoa maoni yake, hilo linaonyesha kwamba anapendezwa na mazungumuzo. Ikiwa mutu anafuata usomaji wa maandiko katika Biblia, hilo linaonyesha kwamba anaheshimu Neno la Mungu. Mara nyingi, ni vizuri kumuuliza mutu ikiwa atasoma kichapo tunachomutolea. Wahubiri wanapaswa kutumia akili ili kujua ikiwa mutu anapendezwa kwelikweli. Kwa mufano, tunapohubiri barabarani, si jambo lenye kufaa kutoa ovyoovyo magazeti, broshua, ao vitabu kwa kila mutu anayepita. Ikiwa hatuko hakika kwamba mutu anapendezwa ao hapana, ni vizuri kumutolea mwaliko ao trakti.

Vivyo hivyo, katika kutaniko, muhubiri atapewa vichapo anavyohitaji kwa ajili ya kazi ya kuhubiri hata ikiwa hana uwezo wa kutoa michango. Michango haitolewi ili kununua vichapo, lakini inatolewa ili kutegemeza sehemu zote za kazi ya kuhubiri ulimwenguni pote. Hata iwe tuna mapato mengi ao kidogo, kutambua kwamba vichapo vyetu ni vya maana kutatuchochea kutoa michango ili kutegemeza kazi ya Ufalme kulingana na mapato yetu. (Marko 12:41-44; 2 Kor. 9:7) Pia, kutambua kwamba vichapo vyetu ni vya maana kutatuchochea tuchukue tu vichapo tunavyohitaji, kufanya hivyo kutaonyesha kwamba tunatumia vizuri feza zilizotolewa ili kulipia garama ya vichapo.

[Wazo la fungu kwenye ukurasa 2]

Wahubiri wanapaswa kutumia akili ili kujua ikiwa mutu anapendezwa kwelikweli

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine