Utoaji Mbalimbali Uliopendekezwa kwa Ajili ya Kutoa Kitabu Mkaribie Yehova
◼ Ukiwa na Biblia mkononi, sema: “Watu wengi wanaoamini Mungu wangependa kujisikia kuwa karibu zaidi naye. Je, ulijua kwamba Mungu anatualika tumkaribie? [Soma Yakobo 4:8.] Kichapo hiki kilifanywa ili kusaidia watu watumie Biblia yao wenyewe ili kumkaribia Mungu.” Soma fungu la 1 kwenye ukurasa wa 16.
◼ Ukiwa na Biblia mkononi, sema: “Leo ukosefu wa haki ni mwingi. Ni kama tu inavyoelezwa hapa. [Soma Mhubiri 8:9b.] Wengi hujiuliza hata ikiwa Mungu anajali. [Soma sentensi mbili za kwanza za fungu la 4 kwenye ukurasa wa 119.] Sura hii inaeleza kwa nini Mungu ameruhusu ukosefu wa haki kwa muda.”