Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 2/04 uku. 6
  • Faidika Kutokana na Kujifunza Kitabu Mkaribie Yehova

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Faidika Kutokana na Kujifunza Kitabu Mkaribie Yehova
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2004
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Tutaanza Kujifunza Kitabu Mkaribie Yehova Juma la Tarehe 6 Mwezi wa 1
    Huduma Yetu ya Ufalme—2013
  • Tujifunze Kitabu Mwabudu Mungu
    Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • Utoaji Mbalimbali Uliopendekezwa kwa Ajili ya Kutoa Kitabu Mkaribie Yehova
    Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • Tutajifunza Kitabu Furaha Ya Familia
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2004
km 2/04 uku. 6

Faidika Kutokana na Kujifunza Kitabu Mkaribie Yehova

1 Kwenye Mkusanyiko wa Wilaya “Watangazaji Wenye Bidii wa Ufalme,” Tulishangilia sana kupokea kitabu Mkaribie Yehova. Wengi walisoma kitabu hicho mara moja walipokipokea. Bila shaka, wengine wengi walichochewa kufanya hivyo na andiko la mwaka 2003: “Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi.”—Yak. 4:8.

2 Katika Machi tutaanza uchunguzi wa kitabu Mkaribie Yehova kwenye Funzo la Kitabu la Kutaniko. Tunawezaje kufaidika zaidi kutokana na funzo letu? Kujitayarisha ni kwa lazima. Kila sura itachukua majuma mawili, na imepangwa kwamba kila juma mafungu machache yachunguzwe kwenye funzo. Hilo litakutolea wakati wa kutosha ili kutoa maelezo yenye kutoka moyoni, yanayotegemea funzo lako na kutafakari juu ya habari mtakayojifunza. Kwa kuongezea, mafungu machache yatachunguzwa katika majuma ambamo sehemu ya kumalizia ya sura inarudiliwa, ili kuacha wakati wa kutumia sehemu inayotofautisha kitabu hiki na vingine.

3 Kuanzia sura ya 2, kisanduku “Maswali ya Kutafakari” kinapatikana karibu na mwisho wa kila sura. Baada ya kuchunguza fungu la mwisho katika sura, mwangalizi wa funzo la kitabu ataomba kikundi kizungumzie kisanduku hicho. Atatia moyo washiriki wa kikundi watoe mawazo yao, akitafuta mambo mazuri ambayo ni matokeo ya kutafakari kwao juu ya Maandiko. (Met. 20:5) Zaidi ya maulizo yanayopatikana katika kisanduku, wakati mwingine anaweza kuuliza maulizo kama yafuatayo: ‘Habari hii inakuambia nini kuhusu Yehova? Inakuwa na uvutano gani juu ya maisha yako? Unawezaje kuitumia ili kusaidia wengine?’ Mradi wake utakuwa wa kufanya maelezo yenye kutoka moyoni yatolewe, si kuulizauliza kikundi mambo madogomadogo kana kwamba anafanya mtihani au mashindano.

4 Kitabu Mkaribie Yehova ni cha pekee. Ijapokuwa vichapo vyote vya “mtumwa mwaminifu na mwenye busara” vinamtukuza Yehova, kusudi kamili la kitabu hiki ni kuzungumzia sifa za Yehova. (Mt. 24:45-47) Ni nafasi yenye kusisimua kama nini iliyo mbele yetu! Tutafaidika sana kutokana na funzo kamili la utu wa Yehova. Funzo hili na litusaidie kumkaribia sana Baba wetu wa mbinguni, na acheni tuwe wenye matokeo zaidi katika kusaidia wengine wafanye vivyo hivyo.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine