Tutaanza Kujifunza Kitabu Mkaribie Yehova Juma la Tarehe 6 Mwezi wa 1
1. Kuanzia juma la tarehe 6 Mwezi wa 1, tutapata nafasi gani ya kumukaribia Yehova?
1 Yehova anataka tumukaribie. (Yak. 4:8) Kwa hiyo, kuanzia juma la tarehe 6 Mwezi wa 1, tutajifunza kitabu Mkaribie Yehova kwenye Funzo la Biblia la Kutaniko. Ili kuonyesha kusudi la kitabu hiki, ukurasa wake wa kwanza unasema hivi: ‘Tukitafakari juu ya namna Yehova anaonyesha sifa zake, namna Yesu Kristo alionyesha sifa hizo kabisa-kabisa, na kujua namna sisi pia tunaweza kuonyesha sifa hizo, tutamukaribia Mungu zaidi.’ Wakati uliopita, makutaniko yalijifunza kitabu hiki kuanzia juma la tarehe 15 Mwezi wa 3, 2004, mupaka juma la tarehe 16 Mwezi wa 5, 2005. Lakini, kwa wahubiri karibu milioni mbili ambao wamekuwa Mashahidi wa Yehova kisha wakati huo, itakuwa mara yao ya kwanza kuchunguza sana sifa nzuri za Yehova. Kwa wale ambao wamekwisha kujifunza kitabu hiki, kukirudilia kutawasaidia wafurahie tena zaidi sifa za Yehova.—Zab. 119:14.
2. Funzo la kitabu Mkaribie Yehova litaongozwa namna gani?
2 Funzo Litaongozwa Namna Gani?: Ndugu anayeongoza ataanza kwa kusema maneno mafupi ya utangulizi. Kwa sababu kitabu hakionyeshe maandiko yanayopaswa kusomwa, ndugu anayeongoza ndiye atachagua maandiko hayo. Ili kujikumbusha, ndugu anayeongoza anaweza kuuliza ulizo moja ao maulizo mawili kisha kila funzo. Ikiwa katika sehemu ya kujifunza muna kisanduku “Maswali (ao maulizo) ya Kutafakari,” kisanduku hiki kitatumiwa ili kujikumbusha. Kama kungali wakati, ndugu anayeongoza atachagua maandiko fulani katika kisanduku na kumuomba musomaji ao mutu mwengine asome. Kisha atauliza maulizo fulani ili ndugu na dada watoe maelezo.
3. Wakati wa funzo tunapaswa kufanya nini? Na kwa sababu gani?
3 Faidika Kabisa na Funzo: Hata kama umekwisha kujifunza kitabu hiki, ni vizuri ujitayarishe mbele ya wakati. Toa maelezo, kwa sababu kufanya hivyo kutamuletea Yehova sifa, kutakusaidia kukumbuka mambo ambayo ulijifunza, na kutaletea ndugu na dada faida. (Zab. 35:18; Ebr. 10:24, 25) Kadiri utaendelea kufikiri sana juu ya sifa nzuri za Yehova, utamukaribia zaidi. (Zab. 77:11-13) Kwa kufanya hivyo, utaazimia kabisa kutii amri zake na utachochewa zaidi kuzungumuza na wengine juu yake.—Zab. 150:1-6.