Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 9/03 uku. 3
  • Tujifunze Kitabu Mwabudu Mungu

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Tujifunze Kitabu Mwabudu Mungu
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Faidika Kutokana na Kujifunza Kitabu Mkaribie Yehova
    Huduma Yetu ya Ufalme—2004
  • Furahia Funzo Letu la Kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2006
  • Funzo la Kitabu la Kutaniko—Kwa Nini Tunalihitaji
    Huduma Yetu ya Ufalme—2004
  • Tutaanza Kujifunza Kitabu Mkaribie Yehova Juma la Tarehe 6 Mwezi wa 1
    Huduma Yetu ya Ufalme—2013
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2003
km 9/03 uku. 3

Tujifunze Kitabu Mwabudu Mungu

Kitabu Mwabudu Mungu wa Pekee wa Kweli kimetayarishwa kuwa kitabu cha kujifunza na wapya baada ya hao kumaliza kujifunza kitabu Ujuzi. Kuchunguza kwetu kichapo hicho kwenye Funzo la Kitabu la Kutaniko kutatufanya kuwa tayari ili kukitumia katika huduma na kutatusaidia kuongeza upendo wetu na uthamini wetu kuelekea Yehova na tengenezo lake. Tunawezaje kufaidika kikamili na funzo letu la kitabu Mwabudu Mungu?

Kuongoza Funzo: Kwa kuwa tutakuwa tukichunguza sura nzima kila juma, waangalizi wa mafunzo ya kitabu wanapaswa kupanga wakati kwa hekima. Watapenda kufupisha mazungumzo kwenye mafungu ya utangulizi ili kuacha wakati mwingi zaidi kwa ajili ya habari ya maana zaidi, ambayo kwa kawaida hutokea baadaye katika sura. Kuzungumzia kwa kifupi kisanduku cha kujikumbusha mwishoni mwa kila funzo kutasaidia wale waliopo walinde akilini mambo makuu.

Maulizo yanayotiwa ndani kwa ajili ya mazungumzo na kutafakari yanapatikana karibu katika nusu ya sura za kitabu Mwabudu Mungu. Mfano unaweza kupatikana kwenye ukurasa wa 48-9. Si lazima maulizo hayo yasomwe kwa sauti kubwa pamoja na mafungu. Mwangalizi wa funzo anapoyachunguza pamoja na kikundi, anapaswa kufanya maandiko yanayotajwa yasomwe na kuzungumziwa ikiwa wakati unaruhusu.

Matayarisho ya Kimbele: Kujitayarisha vizuri kwa ajili ya funzo kunahusisha mengi zaidi ya kupiga kistari tu chini ya majibu. Kutafakari kwa bidii maandiko yaliyotajwa kutatuwezesha kutayarisha, si maelezo yetu tu lakini pia, jambo la maana zaidi, kutayarisha mioyo yetu. (Ezra 7:10) Sote tunaweza kuchangia ili kuwe na badilishano la kitia-moyo kwa kutoa maelezo yetu kwa kiasi.—Rom. 1:11, 12.

Funzo letu la kitabu Mwabudu Mungu litatusaidia kumkaribia Yehova na litatufanya kuwa tayari kusaidia wale wenye mioyo minyofu wajiunge nasi ili kumwabudu yeye. (Zab. 95:6; Yak. 4:8) Sote na tufaidike kikamili na uandalizi huu bora wa kiroho.

[Picture on page 3]

Mwabudu Mungu wa Pekee wa Kweli

Programu ya Funzo Mnamo 2003

Okt.20:sura ya 1

27:sura ya 2

Nov. 3:sura ya 3

10:sura ya 4

17:sura ya 5

24:sura ya 6

Des. 1:sura ya 7

8:sura ya 8

15:sura ya 9

22:sura ya 10

29:sura ya 11

Programu ya Funzo Mnamo 2004

Jan. 5:sura ya 12

12:sura ya 13

19:sura ya 14

26:sura ya 15

Feb. 2:sura ya 16

9:sura ya 17

16:sura ya 18

23:sura ya 19

Machi 1:sura ya 20

8:sura ya 21

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine