Tujifunze Kitabu Mwabudu Mungu
Kitabu Mwabudu Mungu wa Pekee wa Kweli kimetayarishwa kuwa kitabu cha kujifunza na wapya baada ya hao kumaliza kujifunza kitabu Ujuzi. Kuchunguza kwetu kichapo hicho kwenye Funzo la Kitabu la Kutaniko kutatufanya kuwa tayari ili kukitumia katika huduma na kutatusaidia kuongeza upendo wetu na uthamini wetu kuelekea Yehova na tengenezo lake. Tunawezaje kufaidika kikamili na funzo letu la kitabu Mwabudu Mungu?
Kuongoza Funzo: Kwa kuwa tutakuwa tukichunguza sura nzima kila juma, waangalizi wa mafunzo ya kitabu wanapaswa kupanga wakati kwa hekima. Watapenda kufupisha mazungumzo kwenye mafungu ya utangulizi ili kuacha wakati mwingi zaidi kwa ajili ya habari ya maana zaidi, ambayo kwa kawaida hutokea baadaye katika sura. Kuzungumzia kwa kifupi kisanduku cha kujikumbusha mwishoni mwa kila funzo kutasaidia wale waliopo walinde akilini mambo makuu.
Maulizo yanayotiwa ndani kwa ajili ya mazungumzo na kutafakari yanapatikana karibu katika nusu ya sura za kitabu Mwabudu Mungu. Mfano unaweza kupatikana kwenye ukurasa wa 48-9. Si lazima maulizo hayo yasomwe kwa sauti kubwa pamoja na mafungu. Mwangalizi wa funzo anapoyachunguza pamoja na kikundi, anapaswa kufanya maandiko yanayotajwa yasomwe na kuzungumziwa ikiwa wakati unaruhusu.
Matayarisho ya Kimbele: Kujitayarisha vizuri kwa ajili ya funzo kunahusisha mengi zaidi ya kupiga kistari tu chini ya majibu. Kutafakari kwa bidii maandiko yaliyotajwa kutatuwezesha kutayarisha, si maelezo yetu tu lakini pia, jambo la maana zaidi, kutayarisha mioyo yetu. (Ezra 7:10) Sote tunaweza kuchangia ili kuwe na badilishano la kitia-moyo kwa kutoa maelezo yetu kwa kiasi.—Rom. 1:11, 12.
Funzo letu la kitabu Mwabudu Mungu litatusaidia kumkaribia Yehova na litatufanya kuwa tayari kusaidia wale wenye mioyo minyofu wajiunge nasi ili kumwabudu yeye. (Zab. 95:6; Yak. 4:8) Sote na tufaidike kikamili na uandalizi huu bora wa kiroho.
[Picture on page 3]
Mwabudu Mungu wa Pekee wa Kweli
Programu ya Funzo Mnamo 2003
Okt.20:sura ya 1
27:sura ya 2
Nov. 3:sura ya 3
10:sura ya 4
17:sura ya 5
24:sura ya 6
Des. 1:sura ya 7
8:sura ya 8
15:sura ya 9
22:sura ya 10
29:sura ya 11
Programu ya Funzo Mnamo 2004
Jan. 5:sura ya 12
12:sura ya 13
19:sura ya 14
26:sura ya 15
Feb. 2:sura ya 16
9:sura ya 17
16:sura ya 18
23:sura ya 19
Machi 1:sura ya 20
8:sura ya 21