Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 2/03 uku. 5
  • Msaada kwa Wakati Unaofaa

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Msaada kwa Wakati Unaofaa
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Msisahau Wale Ambao Wameacha Kutenda
    Huduma Yetu ya Ufalme—2007
  • Kisanduku cha maulizo
    Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • “Munirudilie”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2020
  • Majibu Kwa Maulizo Yenu
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2003
km 2/03 uku. 5

Msaada kwa Wakati Unaofaa

1 Mtume Petro alipotambua uhitaji wa kutia waamini wenzake nguvu, hangaiko lake kuwaelekea lilimchochea awatolee kitia-moyo na vikumbusha vyenye upendo. (2 Pet. 1:12, 13; 3:1) Alihimiza ‘wale ambao walikuwa wamepata imani’ waendelee kusitawisha sifa za kiroho ili wasipate kuwa “ama wasiotenda ama wasiozaa matunda kuhusu ujuzi sahihi juu ya Bwana wetu Yesu Kristo.” (2 Pet. 1:1, 5-8) Lengo la Petro lilikuwa kuwasaidia wafanye mwito na kuchaguliwa ambako walikuwa wamepokea kutoka kwa Yehova kuwe hakika, ili ‘mwishowe waweze kupatikana naye wakiwa bila doa na bila waa na katika amani.’ (2 Pet. 1:10, 11; 3:14) Kwa wengi, kitia-moyo chake kilionekana kuwa msaada kwa wakati unaofaa.

2 Leo, waangalizi Wakristo wanahangaikia watu wa Mungu kwa njia hiyohiyo. Katika hizi “nyakati za mwisho zilizo ngumu kushughulika nazo,” watumishi wengi wa Yehova wanapaswa kupambana na hali zenye kujaribu. (2 Tim. 3:1) Kwa sababu ya matatizo ya sasa ya kiuchumi, ya kifamilia, au ya kibinafsi, wengine wanaweza kuhisi kama alivyohisi Daudi: “Kwa maana mabaya yasiyoweza kuhesabika yamenizunguka, maovu yangu yamenipata hata siwezi kutazama juu; yamezidi kuliko nyole za kichwa changu, na moyo wangu umeniacha.” (Zab. 40:12) Mikazo hiyo inaweza kuwa mikubwa sana kwa kiasi cha kufanya watu hao wapuuze mambo ya maana ya kiroho na kuacha kushiriki katika huduma ya Kikristo. Lakini, ijapokuwa matatizo yao, ‘hawakusahau maagizo ya Yehova.’ (Zab. 119:176) Sasa ndio wakati unaofaa kwa wazee kutolea watu hao msaada unaohitajiwa.—Isa. 32:1, 2.

3 Ili kutosheleza uhitaji huo, wazee wametiwa moyo kufanya jitihada ya pekee ili kusaidia wale ambao kwa sasa hawashiriki katika kazi ya kuhubiri. Ili kutimiza hilo, jitihada kubwa inafanywa sasa na itaendelea mpaka mwezi wa Machi. Waangalizi wa funzo la kitabu wanaombwa kutembelea wale wasiotenda ili kuwatolea msaada wa kiroho wakiwa na lengo la kuwasaidia waanze tena utendaji wao katika kutaniko. Mahali ambapo kuna uhitaji, funzo la Biblia linaweza kupangwa. Wengine wanaweza kuombwa wasaidie. Ikiwa unaalikwa kufanya hivyo, jitihada zako zinaweza kuwa zenye mafaa sana, hasa ikiwa unatoa kitia-moyo kwa fadhili na kwa huruma.

4 Kuna sababu ya kushangilia kwa wote wakati mtu fulani anapoanza tena utendaji wake katika kutaniko. (Luka 15:6) Matokeo ya jitihada zetu za kutia moyo wale wasiotenda yanaweza kuwa “neno linalosemwa kwa wakati wa kufaa.”—Mez. 25:11.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine