Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
MNARA WA MLINZI Aprili 15
“Katika miaka ya karibuni watu wengi wameona kushuka kwa mambo ya thamani ya kiroho. Je, umeona jambo hilo? [Acha mtu ajibu. Kisha soma Zaburi 119:105.] Mambo ya thamani ya kiroho yanaweza kusaidia watu waepuke mitego maishani. Gazeti hili linaonyesha mahali ambapo mambo ya kiroho yaliyo ya thamani kwelikweli yanaweza kupatikana.”
Amkeni! Aprili 22
“Katika ulimwengu wa leo unaoenda haraka, wengi wanajiuliza ikiwa watoto wanakomaa haraka sana. Je, hilo ni hangaiko lako? [Acha mtu ajibu. Kisha soma Mhubiri 3:1, 4.] Kipindi cha utoto hakingepaswa kuwa wakati wa kuletea watu wazima mizigo. Toleo hili la Amkeni! linazungumzia jinsi wazazi wanavyoweza kulinda watoto wao wakati wa kipindi cha utoto.”
MNARA WA MLINZI Mei 1
“Kuna maulizo ambayo wanadamu hawawezi kujibu. Ona mfano huu. [Soma Yobu 21:7.] Je, umepata wakati wowote kuwa na ulizo ambalo ulitaka kuuliza Mungu? [Acha mtu ajibu.] Gazeti hili linaeleza jinsi watu katika sehemu zote za dunia wamepata majibu yenye kutosheleza kwa maulizo matatu ya maana zaidi maishani.”
Amkeni! Mei 8
“Wengi kati yetu wanajua mtu fulani aliye na ugonjwa wa sukari. Je, unajua mengi kuhusu ugonjwa huo? [Onyesha kifuniko cha gazeti, na uache mtu ajibu.] Gazeti hili linazungumzia sababu na jinsi ya kutunza ugonjwa wa sukari. Linazungumzia pia ahadi ya Biblia ya ponyo lenye kudumu kwa magonjwa yote.” Malizia kwa kusoma Isaya 33:24.