Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Apr. 15
“Watu wengine wanafikiri kwamba kila jambo linalotukia maishani, kutia ndani misiba, ni mapenzi ya Mungu. Je, umekwisha kujiuliza kuhusu hilo? [Acha mtu ajibu.] Watu wengi wanajua sala hii. [Soma Mathayo 6:10b.] Mapenzi ya Mungu ni nini kuhusu dunia, na ni wakati gani yatakapotimizwa kikamili? Gazeti hili linatoa jibu la Biblia.”
Amkeni! Apr. 22
“Katika ulimwengu wa leo, watu wengine wanajisikia kwamba hawana tumaini. Je, unajisikia hivyo nyakati fulani? [Acha mtu ajibu. Kisha soma Waroma 15:4.] Watu wengi zaidi wanatambua kwamba kuwa na tumaini ni jambo la maana. Utafurahi kuchunguza sababu saba za Kimaandiko kuhusu tumaini, sababu zinazoonyeshwa katika toleo hili la Amkeni!”
Mnara wa Mlinzi Mei 1
“Katika jitihada za kuboresha jamii ya kibinadamu, viongozi fulani wa kidini wanajihusisha katika siasa. Lakini, ona jambo ambalo Yesu alifanya wakati ambapo watu walitaka kumfanya mfalme. [Soma Yohana 6:15.] Yesu alikaza fikira juu ya kitu fulani kitakacholetea watu faida yenye kudumu. Gazeti hili linazungumzia jambo hilo.”
Amkeni! Mei 8
“Watu wengi wanapambana na matatizo kazini. Wengine hata wanasumbuliwa na wafanyakazi wenzao. Je, ulijua kwamba Biblia ina mashauri yanayoweza kutusaidia ili tupambane na matatizo hayo? [Acha mtu ajibu. Kisha soma Methali 15:1.] Gazeti hili linatoa mapendekezo yenye kutumika kuhusu jinsi ya kudumisha amani na wengine kazini.”