Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Mac. 15
“Wengi wetu tumekwisha kupatwa na jambo baya la kufiwa na mtu tuliyempenda. Je, wewe unajua vizuri ahadi hii yenye kufariji? [Soma Matendo 24:15. Kisha acha mtu ajibu.] Hata hivyo, wengi wanajiuliza ni nani watakaofufuliwa? Hilo litatukia wakati gani? Na mahali gani? Gazeti hili linatoa majibu ya Kibiblia kwa maulizo hayo.”
Amkeni! Mac.
“Watu wengi wanaamini kwamba Yesu ni Mungu. Jambo lenye kupendeza ni kwamba Petro mwanafunzi wa Yesu alimtambulisha kuwa Mwana wa Mungu. [Soma Mathayo 16:16.] Je, unafikiri kwamba inawezekana Yesu awe Mungu na wakati huohuo awe Mwana wa Mungu? [Acha mtu ajibu.] Habari katika gazeti hili kwenye ukurasa wa 12-13 inazungumzia ulizo hilo, ikitoa maoni ya Biblia.”
Mnara wa Mlinzi Apr. 1
“Usemi huu wenye kujulikana vizuri unakazia umaana wa kujitwalia ujuzi wa Mungu. [Soma Mathayo 4:4.] Hata hivyo, watu wengi wanaona kuwa jambo gumu kuelewa Neno la Mungu. Je, umekuwa na maoni hayo pia? [Acha mtu ajibu.] Gazeti hili linatoa mapendekezo yanayofaa yanayoweza kukusaidia uelewe Biblia.”
Amkeni! Apr.
“Watu wengi wanajitahidi kupata furaha, lakini inaonekana kwamba ni wachache tu ndio wanaoipata. Je, unafikiri kwamba lolote kati ya mambo yanayoorodheshwa hapa lingesaidia watu kuwa na maisha yenye furaha? [Onyesha kisanduku kwenye ukurasa wa 9. Kisha soma moja kati ya maandiko yanayotajwa.] Toleo hili la Amkeni! linazungumzia hatua zinazotegemea Biblia ili kupata furaha ya kweli.”