Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi 01/03/08
“Kila siku, tunasikia habari kuhusu mateso, magonjwa na kifo. Je, unajiuliza ikiwa siku moja tutaokolewa kutokana na mambo hayo yote? [Acha mtu ajibu.] Andiko hili la Biblia limetolea mamilioni ya watu tumaini. [Soma Yohana 3:16.] Kichwa cha gazeti hili ni ‘Jinsi Kifo cha Yesu Kinavyoweza Kukuokoa.’
Amkeni! Mwezi wa 3
“Je, unafikiri kwamba kuamini mambo yasiyo ya kweli yanayohusiana na desturi za mababu (superstition) kuna hatari ao hapana? [Acha mtu ajibu.] Biblia inatoa maelezo haya yenye kupendeza. [Soma Isaya 65:11.] Habari hii inazungumzia ikiwa kuamini mambo yasiyo ya kweli yanayohusiana na desturi za mababu kunapatana na mafundisho ya Biblia.” Onyesha habari inayoanzia kwenye ukurasa wa 10.
Mnara wa Mlinzi 01/04/08
“Je, ungependa kuona unabii huu ukitimizwa? [Soma Isaya 2:4. Kisha acha mtu ajibu.] Ona kwamba Mungu ataingilia kati ya mambo ya wanadamu na ‘kunyoosha mambo.’ Biblia inaonyesha kwamba Mungu atapigana vita inayoitwa Har-Magedoni, vita itakayomaliza vita vyote. Gazeti hili linaeleza Har-Magedoni ni nini na kwa nini tunapaswa kuingojea kwa hamu.”
Amkeni! Mwezi wa 4
“Je, unafikiri kwamba labda tunaishi katika kipindi cha wakati chenye kuelezwa katika andiko hili? [Soma 2 Timotheo 3:1-4. Kisha acha mtu ajibu.] Kuna sababu nzuri ya kuwa waangalifu sana kuhusu siku za mwisho kwa sababu kutokea kwazo kunaonyesha kwamba mambo mazuri yanangojea dunia. Gazeti hili linaeleza mambo hayo.”