Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi 01/04/08
“Kwa kuwa mali za dunia zinatumiwa vibaya, je, umekwisha kujiuliza ikiwa dunia itabaki milele? [Acha mtu ajibu.] Ona ahadi hii yenye kufariji. [Soma Zaburi 104:5.] Habari hii inazungumzia yale ambayo Biblia inasema kuhusu hali ya dunia ya wakati ujao.” Onyesha habari inayoanzia kwenye ukurasa wa 10.
Amkeni! Mwezi wa 4
“Kwa kuwa tuna mambo mengi ya kufanya, wengi wanaona kwamba ni vigumu kupata wakati wa kumwabudu Mungu. Je, ni vigumu kwako pia? [Acha mtu ajibu. Kisha soma Waefeso 5:15-17.] Habari hii inatoa mafasirio yenye kufaa ya Biblia kuhusu kiasi cha wakati na nguvu ambayo Mungu anataka tumtolee.” Onyesha habari inayoanzia kwenye ukurasa wa 20.
Mnara wa Mlinzi 01/05/08
“Watu wengi wanasema kwamba wanaamini tu yale wanayoona. Je, wewe unakubaliana nao? [Acha mtu ajibu. Kisha soma Waroma 1:20.] Gazeti hili linazungumzia sifa kuu tatu za Mungu ambazo tunaweza kuona waziwazi katika vitu alivyoumba na linaeleza jinsi kujua sifa hizo kunavyoweza kutusaidia.”
Amkeni! Mwezi wa 5
“Watu wengi leo wanaogopa wakati ujao. Je, unafikiri kwamba mambo yatazidi kuwa mema, ao yatazidi kuwa mabaya? [Acha mtu ajibu. Kisha soma Ufunuo 21:3, 4.] Gazeti hili linaeleza kwa nini tunapaswa kuwa na uhakika kwamba karibuni Mungu atamaliza matatizo makubwa ambayo yameshinda wanadamu.”