Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Apr. 15
“Leo kiasi cha habari kinachopatikana ni kisicho na mwisho, sivyo? [Acha mtu ajibu.] Hata hivyo, hakuna habari iliyo yenye thamani zaidi kuliko habari inayozungumziwa katika andiko hili. [Soma Yohana 17:3.] Gazeti hili linaeleza maana ya usemi ‘uzima wa milele’ na jinsi tunavyoweza kupata ujuzi unaongoza kwenye uzima huo.”
Amkeni! Apr. 22
“Ijapokuwa huenda Yesu Kristo anajulikana vizuri kuliko mtu yeyote aliyepata kuishi, bado watu wengi wanajiuliza yeye alikuwa nani hasa. Je, ulijua kwamba hata mitume wa Yesu walifikiri juu ya jambo hilo? [Acha mtu ajibu. Kisha soma Marko 4:41.] Gazeti hili linazungumzia yale Biblia inayosema kuhusu Yesu ikiwa yeye alikuwa nani.”
Mnara wa Mlinzi Mei 1
“Mtu tunayempenda anapokufa, ni jambo la kawaida kutaka kumwona mtu huyo tena. Je, unakubaliana na hilo? [Acha mtu ajibu.] Wengi wamefarijiwa na ahadi ya Biblia ya ufufuo. [Soma Yohana 5:28, 29.] Gazeti hili linazungumzia wakati ufufuo utakapotukia na nani hasa watakaofaidika na jambo hilo.”
Amkeni! Mei 8
“Wazazi wengi wanafanya uchaguzi kuhusu yale wanayoruhusu watoto wao kutazama kwenye sinema au televisheni. Je, limekuwa jambo gumu kupata sinema zinazofaa familia yako? [Acha mtu ajibu. Kisha soma Waefeso 4:17.] Gazeti hili linazungumzia jinsi wazazi wanavyoweza kusaidia watoto wao kuchagua viburudisho vinavyofaa.”