Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Mac. 15
“Ulimwenguni pote watu wanasifu mafundisho ya Yesu. [Soma mtajo kwenye ukurasa wa 3, fungu 1.] Lakini je, unafikiri kwamba mafundisho hayo, kama vile mfano unaopatikana katika andiko hili, ni yenye kufaa leo? [Soma Mathayo 5:21, 22a. Kisha acha mtu ajibu.] Gazeti hili linazungumzia mambo ambayo Yesu alifundisha na jinsi tunavyoweza kufaidika kutokana nayo.”
Amkeni! Mac. 22
“Watu wengi wanapenda milima kwa uzuri wayo, lakini, je, ulijua kwamba milima ni ya lazima sana ili kuendeleza uhai duniani? [Acha mtu ajibu.] Gazeti hili linazungumzia kwa nini tunahitaji milima na jambo linaloipata leo. Linaonyesha pia jinsi Muumba atakavyookoa mali hiyo ya maana.” Soma Zaburi 95:4.
Mnara wa Mlinzi Apr. 1
“Je, umewahi kusikia ikisemwa kwamba sayansi na Biblia hupingana? [Acha mtu ajibu.] Gazeti hili linazungumzia historia ya mapambano kati ya sayansi na dini. Lakini linatoa pia uthibitisho ili kuonyesha kwamba sayansi ya kweli inapatana na Biblia.” Onyesha ukurasa 6-7. Kisha soma Mhubiri 1:7.
Amkeni! Apr. 8
“Unafikiri wazazi wanawezaje kusaidia watoto wao kuepuka matatizo mnamo miaka yao ya utineja (ujana)? [Acha mtu ajibu.] Kisha soma Isaya 48:17, 18.] Gazeti hili linaonyesha jinsi kutumia mashauri ya Biblia kunavyoweza kusaidia wazazi waendeleze upashanaji habari mzuri pamoja na watoto wao na kuwatilia mipaka yenye usawaziko.”