Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi 15/03/07
“Mara nyingi watu wanasema kuhusu kuja kwa Yesu Kristo. Je, unafikiri kwamba hilo ni tukio la kungojea kwa hamu au ni tukio la kuogopa? [Acha mtu ajibu.] Ona jinsi mwandikaji wa Biblia Yohana alijisikia kuhusu jambo hilo. [Soma Ufunuo 22:20.] Gazeti hili linazungumzia mambo ambayo yatatimizwa na kuja kwa Yesu.”
Amkeni! Mwezi wa 3
“Viongozi wengi wa ulimwengu wanaonekana kuwa wenye kiburi sana. Je, unafikiri kwamba tabia hiyo inasaidia kuleta amani na upatano katika ulimwengu? [Acha mtu ajibu.] Biblia inasema hivi kuhusu kiburi. [Soma Methali 16:18.] Habari hii inazungumzia faida za kuwa mnyenyekevu.” Onyesha habari inayoanzia kwenye ukurasa wa 20.
Mnara wa Mlinzi 01/04/07
“Karibu kila siku tunapambana na maulizo kuhusu afya yetu, familia yetu na kazi yetu. Unafikiri ni wapi tunaweza kupata majibu yenye kufaa na yenye kutegemeka? [Acha mtu ajibu.] Ona yale ambayo Biblia inasema kwenye 2 Timotheo 3:16. [Soma.] Gazeti hili linaonyesha jinsi Biblia inavyoweza kutusaidia kwa kututolea majibu mbalimbali yenye kufaa.”
Amkeni! Mwezi wa 4
“Katika sehemu nyingi za ulimwengu, watu wanaona kwamba wengi hawaheshimu tena kanuni za mwenendo mzuri. Je, wewe pia umeona jambo hilo? [Acha mtu ajibu.] Hali ambazo tunaona leo zinatimiza unabii wa Biblia. [Soma 2 Timotheo 3:2-4.] Gazeti hili linaonyesha kwa nini watu hawaheshimu tena kanuni za mwenendo mzuri na yale yatakayowapata wanadamu kwa sababu ya hali hiyo.”