Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
MNARA WA MLINZI Mei 15
“Kila siku tunasikia ripoti za jeuri. Je, unafikiri kwamba hali hizo zilipata kuwapo zamani? [Acha mtu ajibu.] Ona yale ambayo Biblia inasema. [Soma Mathayo 24:37.] Siku za Noa zilikuwa mbovu sana hivi kwamba Mungu akaondolea mbali watu wote isipokuwa Noa na familia yake. Gazeti hili linaonyesha jinsi matukio hayo yalivyo na maana kwetu leo.”
Amkeni! Mei 22
“Leo, ugonjwa unaoambukizwa na wadudu ni moja ya mambo yanayotia afya yetu hatarini. Je, ulijua kwamba kuna hatua tunazoweza kuchukua ili kujilinda? [Acha mtu ajibu.] Gazeti hili linazungumzia hatua hizo, na pia ahadi ya Biblia kuhusu wakati ambapo ugonjwa hautakuwapo tena.” Malizia kwa kusoma Isaya 33:24.
MNARA WA MLINZI Juni 1
“Ripoti kuhusu matumizi mabaya ya michango ya fedha zimefanya watu fulani wajiulize ikiwa ni jambo la hekima kutoa michango kwa mashirika ya kutoa misaada. Bado kuna watu wengi walio katika uhitaji. Unafikiri ni jambo gani linaloweza kufanywa? [Acha mtu ajibu. Kisha, soma Waebrania 13:16.] Gazeti hili linaeleza aina ya utoaji unaompendeza Mungu.”
Amkeni! Juni 8
“Inaonekana kwamba leo watu hawathamini maadili na tabia nzuri kama ilivyokuwa katika miaka iliyopita. Je, umeona hilo kuwa kweli? [Acha mtu ajibu.] Kwa kupendeza, Biblia ilitabiri jambo hilo. [Soma 2 Timotheo 3:1-5.] Toleo hili la Amkeni! linazungumzia kwa nini maadili ya kibinadamu yanabadilika na yale ambayo wakati ujao unatuwekea.”