Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Machi 15
“Tungependa kukualika kwenye mwadhimisho wa Mlo wa Jioni wa Bwana, Siku ya Yenga, mnamo Aprili 4. [Eleza kwa kutumia ukurasa wa mwisho wa gazeti hilo au karatasi iliyochapishwa ya mwaliko wa Ukumbusho. Kisha soma Luka 22:19.] Makala za mwanzo katika toleo hili la Mnara wa Mlinzi zinazungumzia maana ya tukio hilo na jinsi linavyoadhimishwa.”
Amkeni! Machi 22
Baada ya kutaja tukio lenye kuhuzunisha lililo katika akili ya watu, uliza: “Je, umekwisha kujiuliza kwa nini Mungu anaruhusu mambo kama hayo yatukie? [Acha mtu ajibu. Kisha soma Yakobo 1:13.] Makala hii, ambayo imeandikwa hasa kwa ajili ya vijana, inaeleza kwa nini Muumba wetu mwenye upendo hajaingilia kati ili kumaliza mateso ya wanadamu.”
Mnara wa Mlinzi Apr. 1
“Kuna maandishi machache ambayo yamekisia kuhusu ufafanuzi wa kifumbo wa Biblia kuhusu alama ya mnyama. Je, umekwisha kusikia juu ya hilo? [Acha mtu ajibu. Kisha soma Ufunuo 13:16-18.] Biblia yenyewe ina funguo ili kutambua maana ya fumbo hilo. Gazeti hili linazungumzia funguo hizo.”
Amkeni! Apr. 8
“Watu wengi wanajua sana simulizi la maisha ya Musa. Lakini, je, unajua kwamba Musa alisema jambo fulani linalohusu maisha yetu leo? [Acha mtu ajibu. Kisha soma Kumbukumbu la Torati 18:15.] Toleo hili la Amkeni! linazungumzia habari inayohusu yule nabii aliyetabiriwa na yale atakayofanya kwa faida ya wanadamu.”