Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 8/04 uku. 5
  • Programu Mpya ya Mkusanyiko wa Mzunguko?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Programu Mpya ya Mkusanyiko wa Mzunguko?
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2004
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Kujikumbusha Mkusanyiko wa Mzunguko
    Huduma Yetu ya Ufalme—2004
  • Programu Ya Kusanyiko Lipya La Mzunguko
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Programu Ya Kusanyiko La Mzunguko Lijalo
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Mkusanyiko wa Mzunguko Ambao Utatusaidia Kulinda Hali Yetu Njema ya Kiroho
    Huduma Yetu ya Ufalme—2009
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2004
km 8/04 uku. 5

Programu Mpya ya Mkusanyiko wa Mzunguko?

Katika hizi “nyakati za hatari zilizo ngumu kushughulika nazo,” tunahitaji hekima ya Kimungu ili kupata na kulinda kibali cha Yehova. (2 Tim. 3:1) Programu ya mkusanyiko wa mzunguko kuhusu mwaka wa utumishi wa 2005 itatutolea mashauri yenye kufaa na vitia-moyo inapozungumzia kichwa “Ongozwa na ‘Hekima Inayotoka Juu.’”—Yak. 3:17.

Sehemu ya kwanza ya hotuba-mfululizo, “Kuonyesha ‘Hekima Inayotoka Juu’ Katika Maisha Yetu,” itatusaidia tuelewe kinachohusika katika kuwa safi kiadili, kuwa wafanya-amani, wenye kusawazika, na tayari kutii. Kisha mwangalizi wa mzunguko ataelekeza uangalifu kwenye mambo mengine matatu kuhusu hekima ya Kimungu. Mwangalizi wa wilaya atamalizia siku ya kwanza kwa kuonyesha jinsi wahudumu Wakristo, ijapokuwa wanaonwa na wengine kuwa “watu wasio na elimu na wa kawaida,” wanapewa vifaa ili wastahili kuzungumzia hekima ya Kimungu.—Mdo. 4:13.

Kwenye siku ya pili, sehemu ya hotuba-mfululizo yenye kichwa “Fuatia Yale Mambo Yanayojenga” itatusaidia kutambua na kuepuka mambo yanayoweza kudhoofisha hali yetu ya kiroho. Itatuonyesha pia jinsi tunavyoweza kujenga wengine kwenye mikutano ya kutaniko, katika utumishi wa shambani, na katika familia yetu. Hotuba ya watu wote: “Jinsi Hekima ya Kimungu Inavyotufaidi” itaongeza shukrani tunayo kwa sababu ya faida tunazopata tunapotumia kanuni za kimungu katika maisha zetu. Hotuba ya kumalizia, “Kutenda Kulingana na Hekima ya Kimungu Kunatulinda,” itatia nguvu azimio letu la kumwendea Yehova ili kupata hekima katika siku hizi za mwisho.

Jambo kubwa kwenye kila mkusanyiko ni ubatizo wa wanafunzi wapya. Shule ya Huduma ya Kitheokrasi na Funzo la Mnara wa Mlinzi la kila juma itakuwa pia kwenye programu. Yehova anatamani sisi wote tufaidike na hekima anayotoa. Tutatajirishwa kiroho na mashauri na vitia-moyo vinavyotungojea kwenye mkusanyiko wetu wa mzunguko.—Met. 3:13-18.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine