Kujikumbusha Mkusanyiko wa Mzunguko
Habari hii itatumiwa ili kuonyesha kimbele na kujikumbusha programu ya mkusanyiko wa mzunguko kuhusu mwaka wa utumishi wa 2005. Makala “Mpango Mpya kuhusu Kujikumbusha Programu za Mikusanyiko,” inayopatikana kwenye ukurasa wa 4 wa nyongeza hii, inaeleza jinsi kujikumbusha huko kunavyopaswa kufanyika. Wakati wa kujikumbusha huko, pangeni wakati ifaavyo ili maulizo yote yachunguzwe. Kujikumbusha kunapaswa kukazia jinsi tunavyoweza kutumia katika maisha habari iliyotolewa.
KIPINDI CHA ASUBUHI [AU CHA KISHA MCHANA-KATI] CHA SIKU YA KWANZA YA MKUSANYIKO
1. Ni nini kitakachotusaidia tupate hekima ya kimungu?
2. Ni jitihada gani wale walio katika mzunguko wetu wamefanya ili kupelekea watu wengi zaidi habari njema?
KIPINDI CHA KISHA MCHANA-KATI [AU CHA JIONI] CHA SIKU YA KWANZA YA MKUSANYIKO
3. Kwa nini ni jambo la maana kwa Wakristo kubaki safi kiakili na kiroho? Hilo linaomba tufanye nini?
4. Tunawezaje kuonyesha kuwa wafanya amani na ndugu zetu?
5. Usawaziko ni nini, na jinsi gani tunavyoweza kuuonyesha katika namna tunayotumia wakati wetu?
6. Tunajifunza nini kutokana na mfano wa Sauli na Noa? Ni katika njia gani tunavyoweza kuonyesha kwamba tuko “tayari kutii”? (Yak. 3:17)
7. Mkristo anawezaje kujilinda na maisha ya namna mbili?
8. Tunawezaje kuiga mfano wa Paulo katika kuzungumzia hekima ya Kimungu?
KIPINDI CHA ASUBUHI CHA SIKU YA PILI YA MKUSANYIKO
9. Kwa nini tunapaswa kuwa waangalifu tunapochagua utendaji tunaofuatia, na nini kitakachotusaidia kufanya hivyo?
10. Ni jitihada gani wale walio katika mzunguko wetu wanafanya ili kuhudhuria mikutano kwa ukawaida, na wamefaidikaje kwa kufanya hivyo?
11. Vichwa vya familia wanawezaje kujenga watu wa nyumba yao?
12. Tulijulishwa kwamba mzunguko wetu unayo mahitaji gani?
KIPINDI CHA KISHA MCHANA-KATI CHA SIKU YA PILI YA MKUSANYIKO
13. Kama ilivyoonyeshwa katika hotuba ya watu wote, ni kazi gani zenye haki ambazo zimetokezwa na hekima inayotoka juu?
14. Kwa nini ni jambo la kipumbavu kujitegemea au kutegemea wale wasioongozwa na hekima ya kimungu? Ni katika mambo gani tunahitaji kuwa macho?
15. Hekima ya Kimungu inatulinda na mitego gani?
16. Kwa nini ni jambo la maana kwetu kutumia mashauri tuliyopokea kwenye programu ya mkusanyiko wa mzunguko?