Kujikumbusha Kusanyiko la Pekee la Siku Moja
Habari hii itatumiwa ili kuonyesha kimbele na kujikumbusha programu ya kusanyiko la pekee la siku moja kuhusu mwaka wa utumishi wa 2005. Makala “Mpango Mpya kuhusu Kujikumbusha Programu za Mikusanyiko,” inayopatikana kwenye ukurasa wa 4 wa nyongeza hii, inaeleza jinsi kujikumbusha huku kunavyopaswa kufanyika. Wakati wa kujikumbusha huku, pangeni wakati ifaavyo ili maulizo yote yachunguzwe. Kujikumbusha kunapaswa kukazia jinsi tunavyoweza kutumia katika maisha habari iliyotolewa.
KIPINDI CHA ASUBUHI
1. Kwa nini kuna uhitaji wa kumsikiliza Yehova zaidi kuliko wakati wowote? Kusikiliza kunamaanisha nini? (Kutokana na habari “Kwa Nini Kusikiliza Sauti ya Yehova”)
2. Familia zinawezaje kudumisha programu nzuri ya utendaji wa kiroho? (Kutokana na habari “Familia Zinazosikiliza Neno la Mungu Bila Kukengeushwa”)
3. Jinsi gani wale walio katika mzunguko wetu wametumia nafasi zilizojitokeza ili kutoa ushahidi wa vivi hivi? (Kutokana na habari “Tufanye Mambo Yote kwa Utukufu wa Mungu”)
4. Ni nini tunayoweza kujifunza kutokana na mfano wenye kuonya unaopatikana katika Waebrania sura ya 3 na 4? Yehova anasemaje nasi leo? (Kutokana na habari “Kusikiliza Mungu Anaposema Kunatulinda”)
5. Ulifaidikaje na hotuba kwa ajili ya ubatizo? (Kutokana na habari “Wakfu na Ubatizo”)
KIPINDI CHA KISHA MCHANA-KATI
6. Ni nini tunaloweza kutambua kuhusu Yesu akiwa kijana, na jinsi gani vijana katika mzunguko wetu wanavyoiga mfano wake? (Kutokana na habari “Jinsi Kusilikiliza kwa Makini Neno la Mungu Kunavyoimarisha Vijana Wetu”)
7. Ni njia fulani gani ambazo katika hizo wazazi wanaweza kuanza kuzoeza watoto katika njia za Yehova? (Kutokana na habari “Watoto Wadogo Wanaomsikiliza Mungu na Kufunzwa”)
8. Ni sehemu gani kamili ambazo katika hizo tunahitaji kutoa uangalifu kwa Yehova, Mwana wake, na “mtumwa mwaminifu na mwenye busara”? (Mt. 24:45) Kwa nini kufanya hivyo ni jambo la maana? (Kutokana na habari “Kazia Uangalifu Daima kwa Maagizo ya Kimungu”)