Programu Mpya ya Kusanyiko la Pekee la Siku Moja
Ikiwa tunaona au kusikia ishara moja yenye kuonya lakini hatutende, matokeo yanaweza kuwa mabaya sana. Ni jambo la maana hata zaidi kufuata mwongozo wa kiroho ambao Yehova anatoa. Hilo litakaziwa katika programu ya kusanyiko la pekee la siku moja la mwaka wa utumishi unaokuja. Kichwa cha kusanyiko hilo ni “Kazieni Uangalifu Jinsi Mnavyosikiliza.”—Luka 8:18.
Katika hotuba yake ya kwanza, msemaji mgeni atachunguza jinsi shauri linalopatikana kwenye sura za utangulizi za barua ya Paulo kwa Waebrania linavyotumika kwetu leo. Katika hotuba ya kumalizia, “Kazia Uangalifu Daima kwa Maagizo ya Kimungu,” msemaji mgeni atasaidia wote kujichunguza ikiwa kweli wanamsikiliza Yehova, Mwana wake, na “mtumwa mwanamifu na mwenye busara.”—Mt. 24:45.
Sehemu nyingi kwenye programu zitafaidi hasa familia. Hotuba “Familia Zinazosikiliza Neno la Mungu Bila Kukengeushwa” itatusaidia kuepuka mambo ya ulimwengu yasisonge hali yetu ya kiroho. Itatia ndani mahojiano ya wale ambao wamefanya mabadiliko ili kutia mambo ya kiroho pa nafasi ya kwanza. Hotuba “Jinsi Kusikiliza Neno la Mungu kwa Makini Kunavyoimarisha Vijana Wetu” itatia ndani mahojiano ya vijana ambao wamechukua msimamo upande wa kweli shuleni, kuhusu wenzao, au katika huduma. Hotuba “Watoto Wadogo Wanaomsikiliza Mungu na Kufunzwa” itatusaidia tusidharau uwezo wa watoto wa kujifunza. Mahojiano pamoja na watoto na wazazi wao itatusaidia kuona faida inayotokana na kufundisha watoto njia za Yehova tangu utoto mchanga.
Huku Shetani akiwa mwenye ‘kuipotosha dunia nzima inayokaliwa,’ Yehova ni mwenye kuonyesha watumishi wake waaminifu njia ambayo katika hiyo wanapaswa kutembea. (Ufu. 12:9; Isa. 30:21) Kusikiliza kwa uangalifu mashauri yake na kuyatumia katika maisha yetu kunatufanya tuwe na hekima, kunatuletea furaha, na kunaongoza kwenye uzima wa milele.—Met. 8:32-35.