Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 8/05 uku. 6
  • Programu Mpya ya Kusanyiko la Pekee la Siku Moja

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Programu Mpya ya Kusanyiko la Pekee la Siku Moja
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2005
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Kujikumbusha Kusanyiko La Pekee La Siku Moja
    Huduma Yetu ya Ufalme—2005
  • Dumisha Jicho Lako Likiwa Rahisi
    Huduma Yetu ya Ufalme—2004
  • Programu Mpya ya Kusanyiko la Pekee la Siku Moja
    Huduma Yetu ya Ufalme—2004
  • Programu mpya ya kusanyiko la pekee la siku moja
    Huduma Yetu ya Ufalme—2000
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2005
km 8/05 uku. 6

Programu Mpya ya Kusanyiko la Pekee la Siku Moja

Jicho liliumbwa kwa njia ya ajabu. (Zab. 139:14) Hata hivyo, linaweza kukaza uangalifu juu ya kitu kimoja tu kwa wakati mmoja. Hilo ni kweli kwa njia halisi na pia kwa njia ya mfano. Ili maono yetu ya kiroho yawe wazi na yawe na lengo, tunapaswa kukazia fikira yetu juu ya kufanya mapenzi ya Mungu. Kwa sababu ya vikengeusha fikira vya ulimwengu wa Shetani vinavyoongezeka, ni jambo lenye kufaa kabisa kwamba programu yetu ya kusanyiko la pekee la siku moja katika mwaka wa utumishi wa 2006 iwe na kichwa “Dumisha Jicho Lako Likiwa Rahisi.”—Mt. 6:22.

Tunaweza kufanya nini ili kupokea baraka kutoka kwa Yehova? (Met. 10:22) Ulizo hilo litazungumziwa katika sehemu yenye kichwa, “Vuna Baraka Kwa Kudumisha Jicho Likiwa Rahisi.” Mahojiano yatakazia jinsi tunavyoweza kufaidika kwa kutumia kanuni za Kimaandiko. Hotuba ya kwanza itakayotolewa na msemaji mgeni yenye kichwa, “Kudumisha Jicho Rahisi Katika Ulimwengu Mwovu,” itatuonya kuhusu mambo ambayo yanaweza kuvuruga maisha yetu na kusonga ukuzi wetu wa kiroho pole kwa pole. Tutafunzwa pia mambo yanayohusishwa katika kuchagua “fungu jema.”—Luka 10:42.

Wazazi na watu wengine wanawezaje kutia moyo vijana Wakristo kukaza fikira juu ya mambo ya kiroho? Sehemu zenye vichwa, “Wazazi Wanaolenga Mishale Yao Sawasawa” na “Vijana Wanaojitahidi Kufikia Miradi ya Kiroho” zitatia ndani maelezo ya wazazi na vijana kuhusu ulizo hilo lenye maana. (Zab. 127:4) Hotuba ya kumalizia itakayotolewa na msemaji mgeni itazungumzia jinsi tunavyoweza kutembea sambamba pamoja na tengenezo la Yehova tukiwa mtu mmoja mmoja, familia, na tukiwa kutaniko.

Iwe sisi ni wapya katika kweli ama tumemtumikia Yehova kwa makumi mengi ya miaka, ni jambo la maana kwamba ‘tudumishe jicho likiwa rahisi.’ Programu ya kusanyiko la pekee la siku moja itatusaidia kufanya hivyo.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine